Shanta gold mine kuanza kumimina dhahabu kuineemesha Ikungi, mbunge Mtaturu afunguka

Shanta gold mine kuanza kumimina dhahabu kuineemesha Ikungi, mbunge Mtaturu afunguka

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
SHANTA GOLD MINE KUANZA KUMIMINA DHAHABU KUINEEMESHA IKUNGI, MBUNGE MTATURU AFUNGUKA

SHANTA gold mine sasa Kumimina Dhahabu kuineemesha Ikungi. Ni baada ya Kusimama kwa muda mrefu takribani miaka 19 tangu kusimama kwake sababu ikitajwa kuwa ni baadhi ya Wanasiasa kuweka vikwazo vilivyomfanya mwekezaji Kuutelekeza mgodi huo.

Akijibu Swali la Mwananchi wa Ikungi aliyeuliza kwa Mkuu wa Mkoa Wa Singida Mhe. Peter Serukamba, ni lini Shanta Gold mine itaanza kufanya kazi na kuwanufaisha wananchi, swali hilo ameliuliza mwananchi katika mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua uliofanyika wilayani hapo Februari 23, 2023 ambapo Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki Mhe. Miraji Mtaturu ameeleza kuwa sasa Mgodi huo utamimina dhahabu na kuineemesha Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kufuatia mapato yatakayopatikana katika Mgodi huo.

Vilevile pia Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Peter Serukamba amesisitiza kuhusu mradi huo wa dhahabu unaotegemewa kuanza kumimina dhahabu kuanzia mwezi March 2023 kwa kuwataka wananchi kujiaandaa kimaendeleo naye alisema. “Ni lazima wananchi Tujiandaae kimaendeleo hii ni fursa kubwa, Halmshauri itapata fedha na mzunguko wa fedha utakuwa mkubwa sana hapa wilayani kwetu, hali ya maisha ya watu itabadilika, lakini niwaombe msiwabeze wawekezaji mtaji wenu wa kwanza wanaikungi ni ardhi yenu”.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Peter Serukamba Februari 23, 2023 amefanya kikao cha kusikiliza kero mbalimbali za Wananchi wa Wilaya ya Ikungi kwa lengo la kuzitatua ambacho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Ziara hii ni muendelezo wa ziara zake za kutembelea Wilaya zote za Mkoa wa Singida kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.07(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.07(1).jpeg
    33.6 KB · Views: 12
  • WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.06.jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.06.jpeg
    29.8 KB · Views: 10
  • WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.08(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.08(2).jpeg
    31.3 KB · Views: 10
  • WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.09(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.09(2).jpeg
    44.2 KB · Views: 13
  • WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.07(2).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-24 at 14.56.07(2).jpeg
    47.1 KB · Views: 9
Tarime na ile North Mara kuna umasikini wa kutisha, pale Musoma Buhema walichimba wakaacha mashimo, Kule Geita kuna nini cha maana pale, Sana sana watafanya danganya toto za kujenga Madarasana na zahanati huku wakizidi kuchimba mahandaki ambayo watakuja kuyaacha
 
Awadanganye wajinga,hii nchi rasilimali wanaofaidi ni wawekezaji na wezi na mafisadi wa ccm
 
Hao Shanta Gold mine mbona tafikiri walikuwa Chunya au ni wale wale kasolo majina
 
SHANTA GOLD MINE KUANZA KUMIMINA DHAHABU KUINEEMESHA IKUNGI, MBUNGE MTATURU AFUNGUKA

SHANTA gold mine sasa Kumimina Dhahabu kuineemesha Ikungi. Ni baada ya Kusimama kwa muda mrefu takribani miaka 19 tangu kusimama kwake sababu ikitajwa kuwa ni baadhi ya Wanasiasa kuweka vikwazo vilivyomfanya mwekezaji Kuutelekeza mgodi huo.

Akijibu Swali la Mwananchi wa Ikungi aliyeuliza kwa Mkuu wa Mkoa Wa Singida Mhe. Peter Serukamba, ni lini Shanta Gold mine itaanza kufanya kazi na kuwanufaisha wananchi, swali hilo ameliuliza mwananchi katika mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua uliofanyika wilayani hapo Februari 23, 2023 ambapo Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki Mhe. Miraji Mtaturu ameeleza kuwa sasa Mgodi huo utamimina dhahabu na kuineemesha Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi kufuatia mapato yatakayopatikana katika Mgodi huo.

Vilevile pia Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Peter Serukamba amesisitiza kuhusu mradi huo wa dhahabu unaotegemewa kuanza kumimina dhahabu kuanzia mwezi March 2023 kwa kuwataka wananchi kujiaandaa kimaendeleo naye alisema. “Ni lazima wananchi Tujiandaae kimaendeleo hii ni fursa kubwa, Halmshauri itapata fedha na mzunguko wa fedha utakuwa mkubwa sana hapa wilayani kwetu, hali ya maisha ya watu itabadilika, lakini niwaombe msiwabeze wawekezaji mtaji wenu wa kwanza wanaikungi ni ardhi yenu”.

Wakati huo huo Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe. Peter Serukamba Februari 23, 2023 amefanya kikao cha kusikiliza kero mbalimbali za Wananchi wa Wilaya ya Ikungi kwa lengo la kuzitatua ambacho kimefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo.

Ziara hii ni muendelezo wa ziara zake za kutembelea Wilaya zote za Mkoa wa Singida kwa lengo la kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.
Kuwaneemesha wahuni wa nchi hii siyo Ikungi, maneno kama hayahaya yalisemwa
Kahama
Geita
Nzega
Tarime
Mererani
Songosongo
Mtwara
Mwisho wa siku tunaishia tozo tozo tozo
 
Back
Top Bottom