Shadida Salum
Journalist at JamiiForums
- Sep 11, 2020
- 69
- 105
Sheffield United ikiwa nyumbani imelazimishwa kichapo cha goli 1 kwa 0 na vijana wa Pep Guardiola, Manchester City katika Dimba la Bramall Lane
Huu ni mwendelezo wa matokeo mabaya kwa Sheffield baada ya kupoteza michezo sita na kusuluhu mchezo mmoja kati ya michezo 7 ambayo imekwisha kucheza tangu msimu kuanza na kushika nafasi ya 19 juu ya Fulham ambaye anashika nafasi ya 20
Klabu hiyo ambayo ilitambuliwa na Shirikisho la Soka Ulimwenguni (FIFA) kuwa klabu kongwe zaidi, ilikuwa na mafanikio makubwa katika msimu wa 2018-2019 na hatimaye kupanda daraja na kushiriki Ligi kuu kwa mara nyingine baada ya kushushwa daraja kwenye Msimu wa 2006-2007
Kwa upande wa Manchester City, imejinyakulia alama 3 katika mchezo huo ambazo hazijaiwezesha klabu hiyo kutoka nafasi moja kwenda nyingine baada ya kuendelea kusalia katika nafasi ya 7 ya msimamo wa ligi hiyo