Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
KUTOKA FB: SHEIKH SULEIMAN TAKADIR ALIVYOPOTEA KATIKA HISTORIA YA UHURU WA TANGANYIKA
Mohamed Said July 11, 2017 0

Mohamed Said Salum Ugomvi kati ya Sheikh Suleiman Takadir na Mwalimu Nyerere ndani ya ofisi ya TANU pale New Street ni katika matokeo ya historia ya TANU ambayo wana TANU wenyewe walipenda labda yafutike yasijulikane.
Nadhani hata Mwalimu Nyerere hakupenda ugomvi ule uingie katika historia yake.
Sheikh Haidar Mwinyimvua
Hakika ni kisa cha kusikitisha. Ugomvi huu alinihadithia marehemu Mzee Haidar Mwinyimvua baba yake Sheikh Ahmed Haidar ambae alikuwapo katika mkutano ule 1958 mara tu baada ya TANU kuamua kuingia katika Kura Tatu.
Dr. Tamim ndiye aliyenipeleka kwa Mzee Haidar nyumbani kwake Magomeni. Alinieleza historia nzima ya Sheikh Takadir na ya Nyerere katika siku zile za mwanzo hadi Sheikh Takadir alipofukuzwa TANU.
Kisa kizima nimekieleza katika kitabu cha Abdul Sykes.
Kushoto ni Sheikh Suleiman Takadir, John Rupia na Julius Nyerere
Mohamed Said Salum Wakati wa utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes sikuweza kupata picha ya Sheikh Takadir popote ikawa kama vile huyu mtu hakuwa katika TANU tena kiongozi wa juu kabisa.
Picha yake ya kwanza nilikuja kuipata miaka hii ya 2000 na alinipa rafiki yangu marehemu Abdallah Kihombo nyumbani kwake Ilala.
Baadae nikapata nyingine kutoka kwa Jim Bailey African Archive, Johannesburg...
Kushoto Julius Nyerere, Sheikh Suleiman Takadiri, Clement Mtamila na Titi Mohamed
Nyuma ya Nyerere, Mama Maria Nyerere, Rajab Diwani na John Rupia
Mohamed Said July 11, 2017 0

Mohamed Said Salum Ugomvi kati ya Sheikh Suleiman Takadir na Mwalimu Nyerere ndani ya ofisi ya TANU pale New Street ni katika matokeo ya historia ya TANU ambayo wana TANU wenyewe walipenda labda yafutike yasijulikane.
Nadhani hata Mwalimu Nyerere hakupenda ugomvi ule uingie katika historia yake.
Sheikh Haidar Mwinyimvua
Hakika ni kisa cha kusikitisha. Ugomvi huu alinihadithia marehemu Mzee Haidar Mwinyimvua baba yake Sheikh Ahmed Haidar ambae alikuwapo katika mkutano ule 1958 mara tu baada ya TANU kuamua kuingia katika Kura Tatu.
Dr. Tamim ndiye aliyenipeleka kwa Mzee Haidar nyumbani kwake Magomeni. Alinieleza historia nzima ya Sheikh Takadir na ya Nyerere katika siku zile za mwanzo hadi Sheikh Takadir alipofukuzwa TANU.
Kisa kizima nimekieleza katika kitabu cha Abdul Sykes.
Kushoto ni Sheikh Suleiman Takadir, John Rupia na Julius Nyerere
Mohamed Said Salum Wakati wa utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes sikuweza kupata picha ya Sheikh Takadir popote ikawa kama vile huyu mtu hakuwa katika TANU tena kiongozi wa juu kabisa.
Picha yake ya kwanza nilikuja kuipata miaka hii ya 2000 na alinipa rafiki yangu marehemu Abdallah Kihombo nyumbani kwake Ilala.
Baadae nikapata nyingine kutoka kwa Jim Bailey African Archive, Johannesburg...
Kushoto Julius Nyerere, Sheikh Suleiman Takadiri, Clement Mtamila na Titi Mohamed
Nyuma ya Nyerere, Mama Maria Nyerere, Rajab Diwani na John Rupia