Sherehe ya kufagia makaburi " qingming festival" wachina wana mambo!

Mto Songwe

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2023
Posts
6,683
Reaction score
14,060
Qingming Festival hii ni sherehe maalumu inayo adhimishwa na jamii ya kichina ulimwenguni kote hasa katika maeneo/nchi zenye jamii kubwa ya kichina mfano China, Indonesia, Thailand, Singapore, Malaysia, Vietnam n.k

Kwa lugha ya kiswahili sherehe hii unaweza kuitambua kama sherehe maalumu ya kufagia makaburi kwa wapendwa wa familia au ukoo.

Utekelezaji wa sherehe hizi umeanza kwa takribani miaka 2000 iliyopita katika jamii za kichina.

Sherehe hii ya kufagia makaburi huusisha pia maombi, ibada mbalimbali kwa wale waliotangulia.

Sherehe hii ni official ndani ya China na Taiwan ila wachina walio katika mataifa mengine huadhimisha kwa kufuata China.

Sherehe hii huangukia katika siku ya 4-6 ndani ya mwezi April ya kila mwaka na mwaka huu 2024 itakuwa 4th April.

Sherehe hii uhusishwa na imani kadhaa mfano kwa wakulima huamini utekelezaji wa tendo la kuwakumbuka waliotangulia kwa kuadhimisha sherehe hii uleta baraka katika mavuno.

Wachina kweli wana mambo!

Mara ya mwisho wewe kufagia kaburi la Babu/Bibi yako na kula chakula kumkumbuka lini ?😄
 
Watu wenye culture zao wako strong. Jamii nyingi za kiafrika tulikopi culture za watu tukatupa za kwetu.
 
Kwa imani yetu kila mwezi wa kumi namoja ni mwezi wa kuwakumbuka marehemu, ibada zote mwezi huo nia kuu ni sala kwaajili ya marehemu, sadaka zote nia ni kwaajili ya kuwaombea Rehema marehemu, hufanyika usafi pia katika makaburi na ibada maalumu huko makaburini kwa nia hio hio ya kuwaombea Rehema, nadhani hatupo mbali na hao wachina.
 
Safi mpo vizuri
 
yani ingekua bongo ningepiga breakfast na lunch makaburini,,,,misosi yote hio aseee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…