SHeria inasemaje kuhusu kukojolea kitabu cha dini?

SHeria inasemaje kuhusu kukojolea kitabu cha dini?

emalau

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2009
Posts
2,775
Reaction score
3,106
Wanajanvi jana asubuhi nilikuwa nikifuatilia matangazo ya Channel 10, nikamuona bwana mkubwa wa nchi akiwapa pole wakiristu ambao makanisa yao yamechomwa moto na kuporwa, Moja ya vitu alivyosema ni kwamba kukojolea kitabu cha dini ni kosa. Ingawa nakubaliana naye kuwa kwa utamaduni tulioujenga wa kuheshimiana na kosa lakini nikajiuliza sheria inasemaje kuhusu hili au iko kimya? Ndo maana nikalitupa hapa janvini waliobobea katika sheria watupe ushauri.

Nawakilisha.
 
wadau wa sheria msaidieni muungwana au kimya ndo tuseme sheria nayo ipo kimya kuhusu hilo swala?
 
Hapa tunatumia Sheria au sharia?
 
Wanajanvi jana asubuhi nilikuwa nikifuatilia matangazo ya Channel 10, nikamuona bwana mkubwa wa nchi akiwapa pole wakiristu ambao makanisa yao yamechomwa moto na kuporwa, Moja ya vitu alivyosema ni kwamba kukojolea kitabu cha dini ni kosa. Ingawa nakubaliana naye kuwa kwa utamaduni tulioujenga wa kuheshimiana na kosa lakini nikajiuliza sheria inasemaje kuhusu hili au iko kimya? Ndo maana nikalitupa hapa janvini waliobobea katika sheria watupe ushauri.

Nawakilisha.

Adhabu ni viboko kumia na viwili .....
 
Kakojolee kitabu cha imani za watu mbele yao halafu utajuwa sheria na hukumu yake.
 
umeleta hoja nzito japo wengi tunaweza kuichukulia kirahisi mkuu.
nafikiri kuna vitu viwili: sheria na kanuni. Kuna mambo ambayo kulingana na mfumo wa maisha yetu haya baadhi ya vitu vinakuja 'automatically' lakini sio kwamba ni sheria. Mfano wote tumezoea kuwa ukitokea masiba jirani unalazimika kushiriki lakini sio lazima. Au tumezoea (wengi wetu) kuwa kazi zinaanza saa mbili asubuhi na kumalizika saa kumi jioni lakini inaweza kuwa tofauti na maeneo mengine ya dunia ambapo nao wana kanuni zao za maisha. Hizi ndizo zuinazaa kanuni ya kuheshimu dini na imani za wengine.
Kitu cha muhimu katika dini ni kuwa mahusianao ya Mungu na Binadamu yako moja kwa moja wala hayapaswi kupitia kwenye kundi au watu fulani ndio yakufikie kama muumini, muhimu ni kusoma Kitabu Kitakatifu alafu anaamua atekeleza vipi zile sheria na ndio maana waumini wa imani moja wanatofautiana katika utekelezaji wa sheria za kiroho. Ikitokea mtu akapiga msitari kuwa kila muumini awe au asishuke (bottom line) 'kiasi fulani cha imani' hapo ni kuingilia kazi ya Mungu.

Kulingana na hoja hii ni bora tukaachana na mambo ya sheria (maana nadhani haiko wazi sana) na kufuata sheria za Vitabu Vitakatifu amabapo vinampa muumini uhuru wa kuviheshimu au kutoviheshimu (it has been left to the individual to decide) na ndio maana kuna mamilioni ya binadamu hawana dini.
Mfano huyo mtoto aliyekojolea Msahafu baada ya kujifunza kutokana na makosa ikitokea kesho akawa muumini safi hata kuwazidi hwa wanaomshambulia itakuwaje??? ...ukichukulia kwamba bila kubishana na mwenzake haya yasingetokea.
Vitabu Vitakatifu vyote vina Ujumbe wa Mungu lakini staili inayotumika kuuwakilisha kwa mhusika ndio inamfanya aukubali au aukatae: jiulize kwa nini wewe ni Muislamu na sio Mkiristo; kwanini ni Mbudha na sio Mkatoriki; ni kwa nini ni mpagani na wakati makanisa, misikiti, mahekalu nk yako wazi??
 
Wanajanvi jana asubuhi nilikuwa nikifuatilia matangazo ya Channel 10, nikamuona bwana mkubwa wa nchi akiwapa pole wakiristu ambao makanisa yao yamechomwa moto na kuporwa, Moja ya vitu alivyosema ni kwamba kukojolea kitabu cha dini ni kosa. Ingawa nakubaliana naye kuwa kwa utamaduni tulioujenga wa kuheshimiana na kosa lakini nikajiuliza sheria inasemaje kuhusu hili au iko kimya? Ndo maana nikalitupa hapa janvini waliobobea katika sheria watupe ushauri.

Nawakilisha.

mimi ninaibandua sheria husika na kuibandika

ni kifungu cha 125 cha Kanunu ya Adhabu cap 16

" Any person who destroys, damages or defiles any place of worship or any object which is held sacred by any class of persons with any intention of insulting the religion of any class of persons or with the knowledge that any class of persons is likely to consider such destruction, damage or defilement as an insult to their religion is gulity of an offence"

wenye lugha zao watafsiri kwa faida ya wote
 
mimi ninaibandua sheria husika na kuibandika

ni kifungu cha 125 cha Kanunu ya Adhabu cap 16

" Any person who destroys, damages or defiles any place of worship or any object which is held sacred by any class of persons with any intention of insulting the religion of any class of persons or with the knowledge that any class of persons is likely to consider such destruction, damage or defilement as an insult to their religion is gulity of an offence"

wenye lugha zao watafsiri kwa faida ya wote
heshima yangu kwa jf inazidi kuongezeka kwa mambo kama haya.
kwa maana hiyo aliyekojolea msaafu ametenda kosa lakini na waliovunja makanisa na magari wana mashitaka ya kujibu pia lakini tofauti ni kuwa mmoja ana miaka 12 lakini wengine ni >18. Sasa napata picha

 
Itabidi itumike sherie inayoshughulika na kudhibiti masuala ya kudhalilisha mtu mwengine.kutukana mtu mwengine au kufanya uchochezi unaohatarisha amani ya taifa.lakini ikithibitika kama muhusika ni mtoto atatakiwa achapwe viboko 10 kila siku kwa muda wa wiki 2;yaani vitano asubuhi na vitano jioni kwa muda wa wiki moja.
 
Sasa hatuelewi yupi aliyekosea zaidi mtoto aliyekojelea kitabu kitakatifu au wakubwa wenye kujua sheria na wakabomoa makanisa?
 
The matter before me is very complicated since the owner of this land has pronounced that this this is a felony offence.How?
 
Aliye fanya hivyo ame fanya kosa kisheria kwani katiba na sheria zi na tambua uwepo wa dini na uhuru wa kuabudu bila kuingiliwa.

Kila mtu yuko huru kuabudu, kwa hiyo inapo tokea mtua ana kashfu au kufanya kitu kibaya juu ya dini ya mwenzie sheria ina fata mkondo.

Kwa huyo ilio fanya hichi kitendo kwanza tutambue ni minor kwa hiyo ata pewa adhabu kulingana na umri wake na pia kuna jela za watoto;pia viboko!

Lakini hii ni defamation

Wanajanvi jana asubuhi nilikuwa nikifuatilia matangazo ya Channel 10, nikamuona bwana mkubwa wa nchi akiwapa pole wakiristu ambao makanisa yao yamechomwa moto na kuporwa, Moja ya vitu alivyosema ni kwamba kukojolea kitabu cha dini ni kosa. Ingawa nakubaliana naye kuwa kwa utamaduni tulioujenga wa kuheshimiana na kosa lakini nikajiuliza sheria inasemaje kuhusu hili au iko kimya? Ndo maana nikalitupa hapa janvini waliobobea katika sheria watupe ushauri.

Nawakilisha.
 
mimi ninaibandua sheria husika na kuibandika

ni kifungu cha 125 cha Kanunu ya Adhabu cap 16

" Any person who destroys, damages or defiles any place of worship or any object which is held sacred by any class of persons with any intention of insulting the religion of any class of persons or with the knowledge that any class of persons is likely to consider such destruction, damage or defilement as an insult to their religion is gulity of an offence"

wenye lugha zao watafsiri kwa faida ya wote

Tujuzeni Kur'ani inasemaje kuhusu mtu asiye Mwislaamu ama asiye na udhu kupokea/kupewa kitabu kitakatifu?
 
SHeria ≠ Sharia and is ≠ to Sheria

:eyebrows::eyebrows::lol::lol:
:deadhorse::deadhorse::deadhorse::deadhorse::deadhorse::deadhorse::deadhorse::deadhorse::deadhorse::deadhorse::deadhorse:
 
Back
Top Bottom