Sheria ya madai Tanzania inawapendelea matapeli?

Sheria ya madai Tanzania inawapendelea matapeli?

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Kwenu wajuvi wa Sheria!

Kwenye clip hapo chini ni malalamiko ya mtu anayedai kutapeliwa. Tukio lilitokea Arusha. Mlalamikaji aliuziwa shamba la ekari 2 kwa milioni hamsini na nne. Lakini alipotaka kuanza kulitumia shamba lake, alilikuta limeuzwa kwa mtu mwingine.

Mtuhumiwa alifunguliwa kesi ya jinai, na baada ya kushindwa mara kadhaa, kesi ilibadilishwa na kuwa ya madai na bado akashindwa. Pamoja na mlalamikaji kushinda, ilibainika kuwa mlalamikiwa hakuwa na mali za kumfidia mlalamikaji. Nyumba yake aliiandikisha familia yake.

Mlalamikaji akaamua kupunguza "machungu" ya kutapeliwa kwa kumfunga gerezani. Lakini huko nako kukawa ni kichekesho.

Utaratibu unamtaka amhudumie mfungwa wake kwa muda wote atakaokuwa gerezani:
1. Kifungua kinywa
2. Mlo wa Mchana na Jioni
3. Maji
Gharama ya mahitaji ya kila siku ni sh 22,000/=

Atahusika pia kumpatia godoro na blanketi, pamoja na kugharamia matibabu yake na mahitaji mengine.

Nitakosea nikisema Sheria ya madai Tanzania inawapendelea matapeli?

Kuna haja ya kuendelea kuwa na Sheria ya vituko kama hiyo?

 
Maana ake akili ichangamke sio unatapeliwa kizembe zembe, uwezi deal nae papendicular
 
Maana ake akili ichangamke sio unatapeliwa kizembe zembe, uwezi deal nae papendicular
Tunatofautiana uelewa mkuu. Hujawahi kutumiwa sms za kitapeli, mfano: "tuma kwenye hii namba..."?

Ni kwa sababu hiyo "biashara" inawahamasisha kuendelea nayo. Inawezekana kuna watu wanaoingia kwenye kumi na nane zao.
 
Kwenu wajuvi wa Sheria!

Kwenye clip hapo chini ni malalamiko ya mtu anayedai kutapeliwa. Tukio lilitokea Arusha. Mlalamikaji aliuziwa shamba la ekari 2 kwa milioni hamsini na nne. Lakini alipotaka kuanza kulitumia shamba lake, alilikuta limeuzwa kwa mtu mwingine.

Mtuhumiwa alifunguliwa kesi ya jinai, na baada ya kushindwa mara kadhaa, kesi ilibadilishwa na kuwa ya madai na bado akashindwa. Pamoja na mlalamikaji kushinda, ilibainika kuwa mlalamikiwa hakuwa na mali za kumfidia mlalamikaji. Nyumba yake aliiandikisha familia yake.

Mlalamikaji akaamua kupunguza "machungu" ya kutapeliwa kwa kumfunga gerezani. Lakini huko nako kukawa ni kichekesho.

Utaratibu unamtaka amhudumie mfungwa wake kwa muda wote atakaokuwa gerezani:
1. Kifungua kinywa
2. Mlo wa Mchana na Jioni
3. Maji
Gharama ya mahitaji ya kila siku ni sh 22,000/=

Atahusika pia kumpatia godoro na blanketi, pamoja na kugharamia matibabu yake na mahitaji mengine.

Nitakosea nikisema Sheria ya madai Tanzania inawapendelea matapeli?

Kuna haja ya kuendelea kuwa na Sheria ya vituko kama hiyo?

View attachment 2997145
HII SHERIA YA KIPUMBAVU INALINDWA NA WAPUMBAVU WA CCM MCHANA NA USIKU NDIYO MAANA NILIWAAMBIA WAPUMBAVU WANASHERIA KUWA KUNA TOFAUTI KATI YA NENO SHERIA NA HAKI ....WAO WANADHANI SHERIA NDIYO HAKI .....NDIYO MAANA WANADHIHILISHA UPUMBAVU WAO ULIO TUKUKA KWA KAULI MBIU YA ...."TUNATAKA UTAWALA WA SHERIA" AU WANASEMA ..."KUTII SHERIA BILA SHURUTI"...misemo hii yote haiwezi kutoka kinywani mwa mtu mwenye akili isipokuwa vinywani mwa watu walio tukuka katika upumbavu.
 
Back
Top Bottom