Shibuda na Peter Serukamba wanataka muungano wa serikali 2 ili kudumisha,undugu,mshikamano na umoja

Shibuda na Peter Serukamba wanataka muungano wa serikali 2 ili kudumisha,undugu,mshikamano na umoja

gogo la shamba

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2013
Posts
6,669
Reaction score
2,165
Ndugu wanajamii katika kipindi cha TBC leo asubuhi,Shibuda na Serukambwa wanasisitiza kwamba,serikali mbili ndizo zinazotufaa kwa kuwa sisi ni wamoja hasa kwa jinsi mahusiano yetu yalivyoingiliana kuanzia kuoana,biashara NK.

Lakini mimi kama Gogo la Shamba nawashangaa sana kama wanayoyasema ni ya kweli kwa nini wasitake serikali moja?Kwa sababu wanazozisema wao ingestahili watake serikali moja,wanachoogopea kusema serikali moja ni kwa sababu wazanzibar hawaitaki serikali moja kwa kuwa hawataki serikali ya Zanzibar ipotee kuliko serikali ya Zanzibar ipotee wako tayari muungano ufe,sasa mimi nauliza kwa wale ambao pia hawapendi serikali ya Tanganyika ife unawapeleka wapi?

Mimi nionavyo hapo la msingi ni serikali tatu ili kila mmoja awe na serikali yake alafu kuwe na serikali ya ubia kati ya Tanganyika na Zanzibar au kama mapenzi yetu ni sawa basi zote tukubali serikali zetu zife tuwe na serikali moja ya muungano. Hebu wanajamii tuchangie hapo kwa kutoa sababu zinazokubalika tusifuate ushabiki.

Naomba kutoa hoja.
 
Naunga mkono serikali moja daima ila kama imeshindikana basi twende kwenye mbili ila tatu majanga.
 
Kwa mtu mwenye akili nyingi, upeo, uelewa na nia njema atataka serikali moja!
 
Watanzania walishaamua mfumo wa serikali TATU,kwenye rasimu ya jaji Warioba ,hizi nyingine ni porojo tu kama za kwenye vikao vya kahawa!


Serikali TATU ,HAZIEPUKIKI!
 
Hivi hao vichaa hawawezi kusikilizwa hata na watoto wa chekechea.
 
siwaseme kweli tu. Wanataka serikali mbili kudumisha ulaji wao.
 
wapendwa katika bwana,hakuna anayekataa muungano usiwepo,si kweli bali watu wanataka Tanganyika huru.Tanganyika kamwe haiwezi kumezwa na muungano.tunahitaji Tanganyika iwe na bendera,katiba,wimbo wake,kiongozi wake mkuu atakayeisemea Tanganyika.kama walivyo Zanzibar.kama haya yanakosekana au kushindikana basi tuwe na serikali moja tu,pasiwepo Tanganyika au Zanzibar.Tanganyika tunahiitaji kuliko tunavyohitaji Zanzibar.
 
Serikali Moja pekee ndio mwisho wa matatizo katika umoja na amani Tanzania. Hata kiuchumi ni bora zaidi. Pia itawaunganisha Watanzania bila kujali rangi au dini.
 
hivi kweli unachoandika humu kweli uwa unawaza na kufikiri?utambue kuwa Tanganyika tunahiitaji zaidi tunavyohitaji Zanzibar.
 
Mnapooana mnakuwa kitu kimoja lakini kuna mke na kuna mume. Mnaishi, mnazaa maisha yanasonga mbele. Sasa kama ni muungano ni wa nchi mbili zikienda kwa majina ya Tanganyika na Zanzibar kwa hiyo hizi ndio serikali mbili za CCM. Tukisema Tanzania hiyo ni serikali moja!
 
Back
Top Bottom