OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Mstari unaotenganisha Rap na uhuni ni mwembamba sana.
Mimi ni mmoja wa watu wanaopenda zaidi rap kuliko aina yeyote ya mziki. Ili roho yangu isuuzike kusikiliza mziki basi inabidi iwe rap. Zamani nikiwa dogo nilikuwa sipati shida kuupa moyo wangu kile unataka.
Sasa unakuwa bro, kinachosemwa rap ni uhuni inabidi ujitahidi kupunguza. Maana ukiweka rap hapa home na familia muda wowote Nas atatukana fu@#$ck police halafu ionekane dingi hapa hatuna.
Hakuna kitu kinakera kama upo ofisini umeamua kujiboost na ngoma kali za Jah Rule, halafu anakuja mtu anakuuliza bro kumbe na wewe huwa unasikiliza Hip Hop. Au anakuja mgeni hapo ofisini anakuta umeweka rap za Talib Kweli zinazungumzia harakati, halafu huyo mtu anakuangalia mara mbili mbili
Hata kupakia familia kwenye gari basi inabidi ujinyime unaweka zile nyimbo za Israel Mbonyi, ukishawashusha ndio unatia kitu cha Mitaa ya Kati-Imam Abas ft Kiroboto. Usipofanya hivyo utasikia "sasa baba yenu katuwekea mamiziki gani hayo" inabidi kumezea tu kujifanya hujasikia.
Tunaopenda Hip Hop tunabezwa sana, inaonekana tunasikiliza kitu cha hovyo
Mimi ni mmoja wa watu wanaopenda zaidi rap kuliko aina yeyote ya mziki. Ili roho yangu isuuzike kusikiliza mziki basi inabidi iwe rap. Zamani nikiwa dogo nilikuwa sipati shida kuupa moyo wangu kile unataka.
Sasa unakuwa bro, kinachosemwa rap ni uhuni inabidi ujitahidi kupunguza. Maana ukiweka rap hapa home na familia muda wowote Nas atatukana fu@#$ck police halafu ionekane dingi hapa hatuna.
Hakuna kitu kinakera kama upo ofisini umeamua kujiboost na ngoma kali za Jah Rule, halafu anakuja mtu anakuuliza bro kumbe na wewe huwa unasikiliza Hip Hop. Au anakuja mgeni hapo ofisini anakuta umeweka rap za Talib Kweli zinazungumzia harakati, halafu huyo mtu anakuangalia mara mbili mbili
Hata kupakia familia kwenye gari basi inabidi ujinyime unaweka zile nyimbo za Israel Mbonyi, ukishawashusha ndio unatia kitu cha Mitaa ya Kati-Imam Abas ft Kiroboto. Usipofanya hivyo utasikia "sasa baba yenu katuwekea mamiziki gani hayo" inabidi kumezea tu kujifanya hujasikia.
Tunaopenda Hip Hop tunabezwa sana, inaonekana tunasikiliza kitu cha hovyo