KERO Shida ya umeme Kimara Kilungule

KERO Shida ya umeme Kimara Kilungule

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BUGE

Senior Member
Joined
Sep 22, 2013
Posts
173
Reaction score
46
Habari viongozi na wadau wa TANESCO, hii shida narudia tena kuitandika hapa, njia hii ya umeme kutoka kimara baruti kwa miaka mingi haishi matatizo, toka enzi zile transfoma ipo juu hadi ikashushwa chini na mafundi wetu kidogo hali ikabadilika, likaja tatizo la umeme kupungua, ikawekwa transfoma nyingine pale darajani hali ikaimarika, sasa hivi tena shida imerudi tena, tena kubwa, ikifika saa 1 usiku umeme ni afadhali ya kibatari, kuunguza vitu ndio kila kukicha, tunaomba mtusaidie maana hali sio nzuri, umeme unasaidia vitu vingi, ikiwemo watoto kusoma n.k.

Nashauri jioni timu ya emergency ipite muda huo wa saa 1 hadi saa 4 wajionee taa zinamulika afadhali ya vibatari.

Asanteni

Naomba kuwasilisha
 
Back
Top Bottom