KERO Shida ya upatikani wa Maji eneo la Ubungo Kibangu na maeneo ya Karibu

KERO Shida ya upatikani wa Maji eneo la Ubungo Kibangu na maeneo ya Karibu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Habari wanafamilia wa JF,

Niende moja kwa moja kwenye hoja:

Kumekuwa na shida ya makusudi ya upatikani wa Maji katika eneo la Ubungo Kibangu na maeneo jirani kama Riverside.

Hapo awali maji yalikuwa yakitoka Kwa wiki mara mbili, baadaye ikawa yanatoka siku moja kwa wiki kati ya Ijumaa hadi Jumapili,lakini hivi karibuni maji hayatoki kabisa hadi mwezi mzima, wananchi wa eneo hili wanapata tabu sana, dumu moja la maji ya chumvi ni shilingi 300-500 na maji yasiyo na chumvi ni 1,000-1,500 kwa dumu.

Imekuwa kero kubwa sana, lakini magari ya kuuza Maji yanapishana na inasemekana ni ya kigogo mmoja anayefanya kazi DAWASA na ndiye anayehakikisha maji hayapatikani eneo hili ili afanye biashara.

Kupitia jukwaa hili tunaomba taarifa hii iwafikie wahusika na hasa Waziri wa maji Aweso aweze kuchunguza jambo hili.
 
Hapo tafuta jina la engineer maji wa huko kwenu pamoja na jina la owner wa hayo magari ya maji. Fanya co relation ya hao watu wawili alafu mwaga ugunduzi wako humu ili hata kama Aweso anasoma, ajue anaanzia wapi. Kero yako is very general, itafanyiwa kazi ila kwa kuchelewa.
 
Habari wanafamilia wa JF,

Niende moja kwa moja kwenye hoja:

Kumekuwa na shida ya makusudi ya upatikani wa Maji katika eneo la Ubungo Kibangu na maeneo jirani kama Riverside.

Hapo awali maji yalikuwa yakitoka Kwa wiki mara mbili, baadaye ikawa yanatoka siku moja kwa wiki kati ya Ijumaa hadi Jumapili,lakini hivi karibuni maji hayatoki kabisa hadi mwezi mzima, wananchi wa eneo hili wanapata tabu sana, dumu moja la maji ya chumvi ni shilingi 300-500 na maji yasiyo na chumvi ni 1,000-1,500 kwa dumu.

Imekuwa kero kubwa sana, lakini magari ya kuuza Maji yanapishana na inasemekana ni ya kigogo mmoja anayefanya kazi DAWASA na ndiye anayehakikisha maji hayapatikani eneo hili ili afanye biashara.

Kupitia jukwaa hili tunaomba taarifa hii iwafikie wahusika na hasa Waziri wa maji Aweso aweze kuchunguza jambo hili.
Jamaa yuko busy kukamata makahaba!
 
Aliyekabidhiwa DAWASA baada ya yule engineer amepwaya sana. Naye waziri wa maji ni kama yuko likizo au anapata % kwenye ujinga huo unaofanyika.
 
Back
Top Bottom