Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Mhe. Eric Shigongo, ametoa kiasi cha fedha shilingi milioni 10 kusaidia kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Majengo, Kata ya Ilenza, ambayo ujenzi wake ulikwama kwa takriban miaka 15.
Akiwa kijijini hapo Machi 07, 2025 Shigongo amewahimiza wakazi wa Kijiji cha Majengo na Buchosa kwa ujumla kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo, akisisitiza kuwa ushirikiano wa jamii ni muhimu kwa mafanikio ya miradi mbalimbali.
Ameeleza kuwa ni muhimu kwa jamii kushirikiana katika kuanzisha miradi ili serikali iweze kusaidia kukamilisha na kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi kwa wakati bila kuingiza siasa kwenye mambo ya msingi kama afya za watu
Mbunge wa Jimbo la Buchosa, Mhe. Eric Shigongo, ametoa kiasi cha fedha shilingi milioni 10 kusaidia kukamilisha ujenzi wa Zahanati ya Kijiji cha Majengo, Kata ya Ilenza, ambayo ujenzi wake ulikwama kwa takriban miaka 15.
Akiwa kijijini hapo Machi 07, 2025 Shigongo amewahimiza wakazi wa Kijiji cha Majengo na Buchosa kwa ujumla kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo, akisisitiza kuwa ushirikiano wa jamii ni muhimu kwa mafanikio ya miradi mbalimbali.
Ameeleza kuwa ni muhimu kwa jamii kushirikiana katika kuanzisha miradi ili serikali iweze kusaidia kukamilisha na kuhakikisha huduma zinawafikia wananchi kwa wakati bila kuingiza siasa kwenye mambo ya msingi kama afya za watu View attachment 3263386
Huyu jamaa hovyo sana. Alikuwa USA sijui kanisani anahamashisha wazungu waombe eti Trump abadili mawazo arudishe misaada aliyoondoa kwa nchi maskini. Ukichunguza utakuta alisafiri kwa business class kwena na kurudi. Uchaguzi unakuja hivyo wengi watajifanya kukumbuka wananchi.