Chukwu emeka
JF-Expert Member
- Jan 12, 2018
- 24,314
- 38,919
Mabingwa mara 27 Tz na mabingwa mara 3 mfulilizo,Yanga leo imeweza kufuzu katika hatua ya makundi ya kombe la shirikisho,japokuwa tumefungwa 1-0, lakini ushindi wa nyumba wa goli 2-0 umekuwa na faida baada ya maana agregate 2-1.Ndani ya miaka miwili Yanga imeweza kufuzu kwa hatua hiyo baada ya mwaka 2016 kufikia hatua hiyo baada ya kuitoa timu ya Sagrada ya Angola kwa matokeo kama haya.Makundi yatapangwa tarehe 21-04-2018,huku Yanga ikiweka kibindoni dola laki 3,sawa na zaidi ya shilling mil 600.
Japo msimu huu Yanga imekuwa na vikwazo vingi ikiwemo wachezaji wengi kuwa majeruhi,ukosefu wa fedha hasa baada ya mfadhili wetu Manji kujiweka pembeni,hali iliyopelekea kutokuwa na matokeo mazuri hata katika ligi ya mabingwa Africa na ligi kuu VPL.Nawapongeza viongozi,wachezaji pamoja na benchi la ufundi bila kuwasahau mashabi na wanachama,kwa umoja na mshikamano hadi kufikia hatua hii ya leo.Msimu huu hata tukikosa ubingwa kufuzu hatua hii itatufuta machozi wan yanga.
Ipo siku kila mtu ataishabikia Yanga,niwaambie tu Simba kuwa karibuni sana pale kwa mchina kuwashabikia wapinzani wetu maana nyie ndo kazi yenu,wenzenu ndo tunasonga ivyo,nyie endeleeni kupiga mziki wa taarabu na MC wenu Hajji Manara,mtajikuta hata VPL linatua Jangwani.
DAIMA MBELE,NYUMA MWIKO
Japo msimu huu Yanga imekuwa na vikwazo vingi ikiwemo wachezaji wengi kuwa majeruhi,ukosefu wa fedha hasa baada ya mfadhili wetu Manji kujiweka pembeni,hali iliyopelekea kutokuwa na matokeo mazuri hata katika ligi ya mabingwa Africa na ligi kuu VPL.Nawapongeza viongozi,wachezaji pamoja na benchi la ufundi bila kuwasahau mashabi na wanachama,kwa umoja na mshikamano hadi kufikia hatua hii ya leo.Msimu huu hata tukikosa ubingwa kufuzu hatua hii itatufuta machozi wan yanga.
Ipo siku kila mtu ataishabikia Yanga,niwaambie tu Simba kuwa karibuni sana pale kwa mchina kuwashabikia wapinzani wetu maana nyie ndo kazi yenu,wenzenu ndo tunasonga ivyo,nyie endeleeni kupiga mziki wa taarabu na MC wenu Hajji Manara,mtajikuta hata VPL linatua Jangwani.
DAIMA MBELE,NYUMA MWIKO