Shilole atamani kuwa Mkuu wa Wilaya ya Igunga, aja na mikakati

Ketoka

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2015
Posts
1,117
Reaction score
1,966
Muimbaji Shilole amezungumza na Ayo TV pamoja na millardayo.com ambapo amesema kuwa anatamani sana siku moja kuteuliwa kuwa mkuu wa Wilaya ya Igunga mahali ambapo ndipo alipotokea, Shishi amesema kuwa anatamani kuiongoza Igunga hata kama kwa nafasi ya Udiwani ili aisaidie na kuiendeleza kwenye mambo mengi.

Shilole amekiri kwamba yeye ndiye mtu aliyeifanya Igunga ikajulikana hivyo ataweza pia kuifanya Igunga ikaendelea kiuchumi na hata kuitangaza zaidi kupitia jina lake.
 
Ajiandae 2020 agombee udiwani.... anajisemesha ili ateuliwe tu from nowhere.

Mwenzie alipambana hakupata bure.
 
tatizo la wanawake ni mpaka wawezeshwe ila kwa nguvu zao hawawezi.
 
Ukuu wa wilaya umekuwa mwepesi siku hizi, njia nyepesi inabidi awe kichaa maana nilisikia hotuba anateua vichaa wenzie.
 
Ilo jambo ni la heri ,raisi wetu askie klio chako akupe uongoz ,ww unafaa sana,ni mtu mtulivu,usiye na makuu ,mpenda watu,mpenda amani,mtu wa watu,unaye jiheshmu sana kwa kutokua na kashfa mtaan,wala kutojiusisha na ujinga wa kutembea na wanaume kla kona,ww ni msanii wa kuigwa na jamii .............
 
Kwani hawezi kuisaidia hiyo Igunga ikaendelea kiuchumi (kama anavyodai) bila ya yeye kua mkuu wa hiyo wilaya?

Nauliza tu!
 
Viongozi wanapaswa kuwa ni wetu wenye hekima,busara,maono maadili na elimu ya kutosha..... lakini pia ni lazima wawe na background nzuri....sio mtu aliyewahi kuwa muhuni au kuishi maisha ya kihuni
 
Ajiandae 2020 agombee udiwani.... anajisemesha ili ateuliwe tu from nowhere.

Mwenzie alipambana hakupata bure.
Alipambana kitandani? Hata yeye vita ya kitandani anaiweza labda hata zaidi ya Joke!
 
mwambieni ajirahisi na amchekeee chekeee jiwe tuu, mambo yatakwenda!!
 
Alipambana kitandani? Hata yeye vita ya kitandani anaiweza labda hata zaidi ya Joke!
Kama kitanda ndio kinampa mtu madaraka basi aongeze sarakasi na chachandu ili kuwashawishi washika dau.
 
Naona tangu mamdogo apate kile cheo,wasanii wanawehuka tu.
Akamuulize mwenzie alifikaje pale ajifunze na yeye
 

Kujiamini ni suala muhimu sana katika maisha. Kama anaona anaweza arudi Igunga kuonesha uwezo na dhamira yake katika kuhudumia WanaIgunga. Wao ndio watambeba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…