Hamjambo.
Tafadhali mnisaidie kueleza kwa ndani zaidi tofauti za matumizi ya maneno yafuatayo:
Shindano/Mashindano - Mchuano/Michuano.
1) Kamusi ya Kiswahili-Kiingereza (TUKI) inatafsiri:
"Mchuano: competition, match"
"Mashindano: 1 competition, contest" ("shindano" halimo)
2) Dictionary of Literary Swahili (Knappert) inatafsiri:
"Mchuano: match, game, contest, encounter"
"Mashindano: 1 contest, competition, race, match" ("shindano" halimo)
3) Comprehensive Swahili-English Dictionary (Mohamed A. Mohamed) inatafsiri:
"Mchuano: contest, match, competition"
"Mashindano: 1 competition, race, contest, match"
"Shindano: contest, competition"
4) Kamusi Kamili ya Kiswahili (Mdee, Shafi, Kiango, Njogu) inafasili:
"Mashindano: 1 mapambano katika mchezo baina ya timu zinazowania tuzo au kikombe fulani" ("shindano" halimo)
"Mchuano: mashindano baina ya timu au wachezaji katika michezo kama vile mchezo wa mpira wa miguu, mpira wa mikono, riadha n.k."
5) Kamusi la Kiswahili Fasaha (BAKIZA) inafasili:
"Shindano: tendo la kupimana uwezo katika jambo k.v. mchezo; makabiliano yenye lengo la kuwania jambo baina ya pande mbili au zaidi" ("mashindano" halimo)
"Mchuano: 2 ushindani k.v. wa kimichezo kati ya timu au mtu na mtu; = mtuano"
Je, mnaweza kutoa mifano ya sentensi zinazotulazimisha tutumie neno fulani badala ya mengine?
Asanteni sana,
Nino
Tafadhali mnisaidie kueleza kwa ndani zaidi tofauti za matumizi ya maneno yafuatayo:
Shindano/Mashindano - Mchuano/Michuano.
1) Kamusi ya Kiswahili-Kiingereza (TUKI) inatafsiri:
"Mchuano: competition, match"
"Mashindano: 1 competition, contest" ("shindano" halimo)
2) Dictionary of Literary Swahili (Knappert) inatafsiri:
"Mchuano: match, game, contest, encounter"
"Mashindano: 1 contest, competition, race, match" ("shindano" halimo)
3) Comprehensive Swahili-English Dictionary (Mohamed A. Mohamed) inatafsiri:
"Mchuano: contest, match, competition"
"Mashindano: 1 competition, race, contest, match"
"Shindano: contest, competition"
4) Kamusi Kamili ya Kiswahili (Mdee, Shafi, Kiango, Njogu) inafasili:
"Mashindano: 1 mapambano katika mchezo baina ya timu zinazowania tuzo au kikombe fulani" ("shindano" halimo)
"Mchuano: mashindano baina ya timu au wachezaji katika michezo kama vile mchezo wa mpira wa miguu, mpira wa mikono, riadha n.k."
5) Kamusi la Kiswahili Fasaha (BAKIZA) inafasili:
"Shindano: tendo la kupimana uwezo katika jambo k.v. mchezo; makabiliano yenye lengo la kuwania jambo baina ya pande mbili au zaidi" ("mashindano" halimo)
"Mchuano: 2 ushindani k.v. wa kimichezo kati ya timu au mtu na mtu; = mtuano"
Je, mnaweza kutoa mifano ya sentensi zinazotulazimisha tutumie neno fulani badala ya mengine?
Asanteni sana,
Nino