Shinyanga: Mbaroni akidaiwa kumuua mama yake mzazi na kufika mwili shambani

Shinyanga: Mbaroni akidaiwa kumuua mama yake mzazi na kufika mwili shambani

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Polisi Mkoa wa Shinyanga limefukua mwili wa Asha Mayenga (62), mkazi wa Lugela, Kata ya Nyamhanga, Manispaa ya Kahama uliofukiwa shambani, baada ya kutoweka kwa siku tano.

Akizungumza na Mwananchi leo Ijumaa, Januari 17, 2025, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Janeth Magomi, amesema mwili huo umekutwa ukiwa umefukiwa jirani na shamba lake la mpunga, lililopo Kijiji cha Malindi, Kata ya Busoka, wilayani humo.

Amesema taarifa za uchunguzi wa awali zinaonyesha mama huyo alikuwa na mgogoro wa shamba na mtoto wake wa kiume.

Soma Pia: Kilimanjaro: Mwanamke mmoja Amuua mama yake mzazi ili arithi shamba

Kamanda amesema Polisi linamshikilia mtoto wa marehemu na wenzake wawili kwa mahojiano kuhusu tukio hilo.

Naye, Mayenga Ng'ombe, mtoto wa marehemu Asha, amedai baada ya ndugu yake (mtuhumiwa) kurejea na kuanza kuhamisha vyombo kwa madai kuwa anahama na kwenda kujitegemea alihisi kuna jambo lisilo la kawaida.
 
Mwaka jana nilipata nafasi ya kutoa mada kwa wazee wastaafu watarajiwa zaidi ya 350 wa taasisi flani. Moja ya ushauri wangu kwa wazee ni kua makini na watoto wao wa kuwazaa kwa sababu mafao hutengeneza aina mpya ya hatarishi kutokea ndani hasa familia.

Kwenye majadiliano hayo ilitolewa mifano mingi sana ya wazee kuuwawa na watoto wao ama wana familia ili wapate access ya urithi. Na hii hatari iko kwa familia za aina zote za vipato, high income to lower income.

Ni mambo ya ajabu sana na ya kusikitisha sana.
 
Yaani unahangaika miezi tisa yote unateseka kwa uchungu masaa kadhaa unajifungua kwa maumivu tele tena unajikuta umeongezewa njia,unafurahia umeleta kidume duniani kumbe ndo kiumbe kitakachokatisha ndoto zoote kisa mali daah
ila kuzaa🙌🏾🙌🏾
 
Yaani unahangaika miezi tisa yote unateseka kwa uchungu masaa kadhaa unajifungua kwa maumivu tele tena unajikuta umeongezewa njia,unafurahia umeleta kidume duniani kumbe ndo kiumbe kitakachokatisha ndoto zoote kisa mali daah
wengine kuzaa kwa operation,unauguza kidonda huku kenyewe kanasumbua usiku kucha,unanyonyesha hadi chuchu zinatoa vidonda,,uuuwiiiii Mungu atusaidie.
 
Back
Top Bottom