Shirika la Bunge la Morocco lapendekeza wanawake kupewa likizo ya hedhi

Shirika la Bunge la Morocco lapendekeza wanawake kupewa likizo ya hedhi

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Kundi la Bunge la Morocco limependekeza mswada utakaowaruhusu wanawake kupewa siku za likizo ya hedhi yenye malipo.

Katika kile ambacho kitakuwa sheria ya aina yake kwa eneo la Mashariki ya Kati na Kaskazini mwa Afrika, pendekezo la kikundi cha haki za kijamii cha shirika la Bunge la Morocco, linalenga kuboresha hali ya wanawake kazini, kupitia utoaji wa likizo ya hedhi yenye malipo ya siku mbili.

Kulingana na mswada uliopendekezwa, wafanyikazi wa kike hawatahitaji kutoa ushahidi wa matibabu kila wakati wanapohitaji kuwa nyumbani.

Mswada huo hata hivyo unahitaji kujadiliwa na kuidhinishwa na serikali ya Morocco.

Wazo iwapo muswada huo utapitishwa, ni kuutekeleza kwa awamu, kuanzia kwa watumishi wa Serikali, ili kuona jinsi utakavyokuwa na ufanisi.

Viongozi hao pia wanaeleza kuwa hedhi ni mwiko ndani ya jamii na kwamba kundi hilo la wabunge linalenga kufungua mjadala kuhusu njia za kuondoa vikwazo vyote vinavyowakabili wanawake katika maisha ya umma.

Iwapo itapitishwa, Morocco itakuwa nchi ya pili barani Afrika, baada ya Zambia, kuwa na sheria hiyo.

Nchi hiyo ya Kusini mwa Afrika ilipitisha sheria hiyo mwaka 2015, inayowaruhusu wanawake kuchukua siku ya mapumziko katika kipindi chao cha hedhi. Nchi nyingine zinazotoa likizo ya malipo ya hedhi ni pamoja na Korea Kusini, Japani, Taiwan na Indonesia.

Chanzo: BBC
 
Kwahiyo kila mwezi kazini wanakuwa wanajua tayari[emoji848][emoji848][emoji848]
Ni nzuri tho.
Ndo maana yake!

Halafu kumbe hadi huku unatembeleaga my dada, ila safi sana

Mwenzio siku hizi niko huku sana tu, navizia fursa ya kwenda Urusi au Ukraine kupiga kazi. Nasikia wana upungufu mkubwa wa wafanyakazi sababu ya vita

Nitarudi kumringishia midolali my dota wako Heaven Sent
 
Ndo maana yake!

Halafu kumbe hadi huku unatembeleaga my dada, ila safi sana

Mwenzio siku hizi niko huku sana tu, navizia fursa ya kwenda Urusi au Ukraine kupiga kazi. Nasikia wana upungufu mkubwa wa wafanyakazi sababu ya vita

Nitarudi kumringishia midolali my dota wako Heaven Sent
Unanywea chai kwenye kikombe au kwa semosi?🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom