KERO Shirika la ndege la Air Tanzania lijitafakari, haliwatendei haki wateja wake

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Joined
May 4, 2024
Posts
19
Reaction score
23
Wakuu,

Leo nimetoka Mwanza kwenda Nairobi kwa ndege ya Air Tanzania. Ndege hizi zinakera sana.

Kwanza kutoka Mwanza ilichelewa kwa nusu saa. Tukavumilia

Kasheshe imetokea tena usiku huu hapa uwanja wa Mwalimu Nyerere. Fikiria ndege ilipaswa kuondoka saa 2 usiku, wakasema itakawia mpaka saa 4 usiku. Robo saa kabla ya kuondoka wanasema itaondoka saa 8 usiku. Kama nchi tupo serious na biashara hii kweli?

Sisi wengine tunaconnection ya ndege na tayari tumeshachelewa. Tutafikaje tunakoenda, hasara hii nani atafidia?

Inakuwaje taarifa ya sitisho la safari inatolewa robo saa kabla ya ndege kuondoka? Maswali ni mengi kuliko majibu.

Serikali ijitafakari, mtasingia kuhujumiwa bure kumbe mnaua biashara wenyewe.

Nimechoka sana kama jina langu lilivyo.

Pia soma: KERO - ATCL imulikwe huenda kuna hujuma, ratiba za safari zao hazieleweki
 
Pole sana kaka. Saiv kila mtu jorowe

Mama kila kila siku safari atayajuaje ya ndani?
 

Hiyo unapanda tu unapoingia nchini toka kenya si ya kupanda kwenda nje kama bado una connect flight zingine huko mbele. Route poa ambayo hawachelewi ni ile ya Uganda. Wako katika muda nyakati zote.
 
Hiyo unapanda tu unapoingia nchini toka kenya si ya kupanda kwenda nje kama bado una connect flight zingine huko mbele. Route poa ambayo hawachelewi ni ile ya Uganda. Wako katika muda nyakati zote.
Madhara ya monopoly hayo!
 
Pole sana kaka. Saiv kila mtu jorowe

Mama kila kila siku safari atayajuaje ya ndani?
Akiwa Tanzania ndio atakua anajua zaidi?

Kauli ya kibwege sana hii

With the digital world, hata akikaa Siberia Bado atakua informed

Tatizo ni atc…. Acha kuleta siasa kila sehemu
 
Ni kweli. Nilipaswa niwe nimefika ili nipumzike kesho nitekeleze majukumu yaliyonileta huku. Bure kabisa hawa jamaa
Pole sana mkuu

Airline industry ni ngumu sana lakini ni muhimu

Kenya wanateseka kuliko sisi

Let’s hope things will get better
 
Reactions: apk
Akiwa Tanzania ndio atakua anajua zaidi?

Kauli ya kibwege sana hii

With the digital world, hata akikaa Siberia Bado atakua informed

Tatizo ni atc…. Acha kuleta siasa kila sehemu
Acha upuuzi unasikia acha kabisa uchawa wako hapa

Utapakwa wewe mpemba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…