Shirika la Posta jirekebisheni

Shirika la Posta jirekebisheni

Nyikanavome

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2008
Posts
484
Reaction score
178
Nimeagiza mzigo wangu kutoka china kupitia aliexpress na nimeufuatilia kupitia traking number mpaka ukatua dar es salaam tarehe 19-07-2016 lakini mpaka leo sijaupata. Nimejaribu kufuatlia kwenye tawi langu hapa Dar lakini wananiambia haujafika kwao. Nimesubiri mpaka ikabibidi niombe kuongezewa muda wa wa buyer protection ili niweze kubuy time kabla ya kuripoti kuwa sijapata mzigo ili kesi ianze ya kurudishiwa hela au kupatiwa mzigo mwingine.

Tabia hii ya kuchelewesha au kupoteza mizigo ya watu inapoteza imani kwa wauzaji wa mtandaoni kwa sie watanzania, kwa hiyo tunaliomba shirika letu litujengee imani kwenye biashara ya mtandao. Mzigo wenyewe ulikuwa simu, sijui imeshaibwa

Naomba wenye uzoefu wa kufuatilia mizigo posta ambayo ina viashiria vya kupotea watoe uzoefu wao ili unisaidie kufuatilia huo mzigo
 
Ulienda na tracking details Posta na wakashindwa kukusaidia?
 
Posta ya Tanzania Kwa kweli m badilike la sivyo mnaturudisha nyuma sana, tangu nianze kuagiza vitu online miaka mitatu sasa, nimeshapotelewa na vitu viwili. Cha mwisho ni hv mwezi huu!
 
Mbona mnatutisha sisi wageni wa haya Mambo tunaotaka kuagiza vitu
nimeagiza vitu vingi tu na vimefika bila shida ila lilipokuja swala la simu aisee WAMEIPIGA.
 
Back
Top Bottom