Shirika la Posta ladaiwa TSh. Bilioni 54.7, lashindwa kujiendeleza na kukopesheka

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mbunge wa Jimbo la Mbagala, Abdallah Chaurembo amesema Shirika la Posta kwasasa linadaiwa TSh. Bilioni 54.7 hivyo kushindwa kujiendeleza na pia shirika limeshindwa kukopesheka, tuimbe sana serikali kama ripoti yetu ilivyoeleza tunaomba serikali ilichukue deni hili ili shirika hili la posta sasa liweze kukopesheka.

Your browser is not able to display this video.
Soma, Pia: Shirika la Posta ni taasisi inayojipeleka kaburini
 
Cha ajabu wakipewa Dp world wananchi ndio tunapiga kelele ila kukiwa na uzembe kwenye taasisi hizo hizo tunapiga kimya!!

PPP ndio suluhu maana serikali ya CCM imefeli kabisa
 
Halafu utasikia linatoa gawio serikalini.!
Pumbav sana. Hili shirika lilitakiwa liwe top two kwenye mashirik ynayotoa huduma za mawsiliano nchini. Eti wnkuja wanajeshi wa vietnam na halotel yao na wanapata wateja
 
Mashirika ya umma ni mzigo kwa umma.Ni vile tuna viongozi wasio na uchungu na pesa za umma.
 
Naona kama vile vifurushi wanavyopitisha pale hata mishahara yao havitoshi kuwalipa....
Wamepewa mkongo wataifa hata hakuna mkoa mmoja wanaweza kuutoa kama mfano r
Kwa sasa hivi tozo zao za vifurushi + kodi za zinaendana na kina DHL/UPS wakati hao washindani wapo mbali sana kwa technologia, na usalama

Ushauri;
1. Deni analipiwa anayezalisha, sasa kama wanachozalisha hakitoshi hata kujiendesha, unalipa deni ili watengeneze deni jingine?
2. Wabunge waje na mkakati rasmi wa kuifufua posta kwa kuweka kodi rafiki kwa parcel za kawaida. Mfano mtu alipie gharama za posta + 18% basi.. kwa tozo zilizopo kwa sasa, sioni wakiweza kushindana na private competitor DHL, na wengine (hawafiki mahali)
3. HAWANA UBUNIFU wa kusogeza huduma karibu na watu (kwenye stand zote kubwa za mabasi, viwanja vya ndege nk. wao ndio walitakiwa wapokee bighaa wazitume kwa mabasi lakini ndio hivyo tena....
4. Wabinafsishe ili Sector binafsi iwasaidie kuendesha
 
Reactions: apk
Haya mashirika ya uma ni mzigo mkubwa Kwa serikali, yameandamwa na madeni na uendeshaji uliokosa ufanisi, watu wanakula mshahara Bure tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…