Shirika la reli Tanzania linaongoza kwa kutolipa stahiki za wastaafu

Shirika la reli Tanzania linaongoza kwa kutolipa stahiki za wastaafu

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Wazee wetu waliolitumikia shirika la reli Tanzania kwa jasho na damu asilimia kubwa kwa sasa wamepoteza maisha na wengine wako hoi vitandani na ama wako hoi kimaisha! Serikali kupitia shirika la reli TRC wanatangaza mafanikio ya SGR na kununua vichwa vipya vya train za kisasa na kujenga reli mpya juu ya laana ya machozi ya wazee Hawa !

TRC ni shirika lenye dharau kubwa kwa wastaafu haijapata kutokea ! TRC ni matapeli wa haki za wafanyakazi wao waliostaafu kwa miaka na miaka ! TRC hawana pesa za kuwalipa makomredi Hawa walioendesha hili shirika kwa tabu na kwa mifumo migumu lakini wanapesa za kununua vichwa na mabehewa mapya !

Nimekutana na mzee magelanga syprian 88 akiwa hoi kitandani anadai amefuatilia stahiki zake mpaka sasa ameamua kumuachia Mungu! Watoto hawana pesa ya kumuuguza Wala makazi ya kuishi ilihali analidai shirika zaidi ya mil 144, kwa nini TRC mmekuwa na roho mbaya kiasi hiki ?

Kwanini TRC hamuogopi kukalia jasho la watu? Kwanini TRC mmebaki na fedha za watu mpaka wamekufa na familia zikifuatilia haki zao mnawapiga danadana mpaka wakate tamaa !!

TRC chini ya Masanja Kadogosa mnaweza kuieleza jamii ya watanzania dhamira yenu ni ipi kama sio utapeli wa jasho la watu ? Tuseme ni TRC ama tuseme ni Masanja Kadogosa? Au mnawapiga danadana ili wafe mjilipe wenyewe? Mnafanya makusudi kwa kuwa mnatembea juu v8 hamkanyagi chini ? Vipi mzazi wako wewe Masanja Kadogosa angekuwa anadai usingemlipa? Na wewe ukistaafu utajisikiaje usipolipwa kwa zaidi ya miaka 20!

Laaana iwe juu yenu nyinyi wote mnaokalia mafaili ya wastaafu bila huruma ,Mungu ilaani TRC !!
 
Eleza vizuri. Ni TRC au ni psssf wanaolipa wastaafu?
 
Hela ya kununua mav8 mapya latest edition ipo siku zote lkn kulipa waastafu utaambiwa uhakiki unaendelea.
 
Mambo mengine ndio maana tunapata laana, unakuta hapo posho ya kikao kimoja unalipa hao wastaafu hata 100 stahiki zao.

Upande mwingine unakuta gari budget za magari ya mabosi hapo TRC hata Kwa safari zisizo na tija unalipa hela za hao wastaafu.

Gharama za matumizi ( operation cost) Kwa mwezi ambazo ni unnecessary unaweza Kuta unalipa hao wazee hata 1000.

Mataifa mengine yanaendelea kwa kuheshimu mchango wa kila mtu kwenye ujenzi wa Taifa, kuheshimu na kuwatendea haki wastaafu na wale wote wanaokufa wakilitumikia Taifa, kulipa stahiki hata kwa familia zilizoachwa na waliofikwa na umauti wakitumikia Taifa.

Honour your ancestors, they will honour you.
 
Mambo mengine ndio maana tunapata laana, unakuta hapo posho ya kikao kimoja unalipa hao wastaafu hata 100 stahiki zao.

Upande mwingine unakuta gari budget za magari ya mabosi hapo TRC hata Kwa safari zisizo na tija unalipa hela za hao wastaafu.

Gharama za matumizi ( operation cost) Kwa mwezi ambazo ni unnecessary unaweza Kuta unalipa hao wazee hata 1000.

Mataifa mengine yanaendelea kwa kuheshimu mchango wa kila mtu kwenye ujenzi wa Taifa, kuheshimu na kuwatendea haki wastaafu na wale wote wanaokufa wakilitumikia Taifa, kulipa stahiki hata kwa familia zilizoachwa na waliofikwa na umauti wakitumikia Taifa.

Honour your ancestors, they will honour you.
Yes mkuu ,Kuna time uchungu unakuja unatamani uchukue hata panga
 
Back
Top Bottom