Shirikisho la Soka la Kongo (FECOFOOT) limefungiwa na FIFA kuanzia Februari 6, 2025, hadi itakapotangazwa tena, huku sababu za uamuzi huo zikiwa bado hazijawekwa wazi. Kufuatia kusimamishwa huko, FECOFOOT itapoteza haki zake zote za uanachama kwa mujibu wa Kifungu cha 13 cha Sheria za FIFA, na hatua zaidi zinatarajiwa kutangazwa na mamlaka husika.
Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kongo ndilo shirika linalosimamia soka huko Jamhuri ya Kongo (Congo Brazzaville). Lilianzishwa mwaka wa 1962, ikishirikiana na FIFA mwaka 1964, na CAF mwaka 1966. Linaandaa ligi ya soka ya Kongo na timu ya taifa.
Inabidi tujue chanzo chake? Je ni hali ya usalama? Je ni wanasiasa kuingilia mpira au nini? Hapa Yanga tutawapata Wakongomani wenye vipaji wa bei chee.