shost yuko njia panda


For experiment sio mbaya...ni kujaribu tu halafu baadae tunaandika vitabu about what is right and wrong.
 
siyo issue kubwa... kwani shostito ana umri gani?

Hili ni swali la muhimu, kama shosti wako ana umri uliosogea kidogo nadhani achukue ngoma hiyo la umri bado ni teenager mshauri asubiri, ya nini kuitafuta eda ndani ya umri mdogo?!
 
Mmh nini kilisababisha wake zake wote wawili kurest in peace??something is wrong somewhere! Shost yeye haogopi kurest in peace?

km umesoma post zangu nimeeleza, kwan mtu akifiwa na wakeze hana haki kuoa?
 

nahc maamuz binafs na mapenzi vinachangia!
 

Mimi attention yangu ni hapo kwenye kufa hapo! Vyema akaangalia vyema, pengne ni roho hizo!
 
Life span yenyewe ka ya mbu, mwambie shost Mwalimu Zawadi anasema...songa songa mbele...songa mbele....wacha watu wakuseme ...we so:A S kiss:nga mbele...
 
Magonjwa yote hayo yanaweza kabisa kuwa na dalili zote za HIV. Awe makini, tena makini sana.

Kuna baba jirani yetu nilivyokuwa mdogo alifiwa na wife wake kwa Cancer miaka ya mid 80s. Wife alipelekwa hadi nje kutibiwa; nywele zilikuwa zimeisha kabisa zikarudi akanawili, lakini baada ya muda akaugua vibaya mno akafa.

Jamaa akaja oa rafiki wa dada zangu; a very beutiful lady; yule second wife akafa ghafla, kwa BP.
Tena huyu second wife alisikitisha sana watu alipoolewa maana alikuwa kwenye serious relationship na kijana mwenzie na alikuwa ndo kwanza kamaliza form four wakati mfiwa alikuwa Capten (pilot); ila jamaa aliyefiwa alikuwa na pesa aswaa; hivyo dada alitaka short cut ya maisha; ambayo ilimpeleka kaburini.

Kaka alomtema sasa hivi ana pesa zaidi ya huyo mfiwa alomuoa.


Watu wakaanza kumuogopa yule mzee; sijuhi kama yuko hai ila watu walianza sema ni HIV case. Alioa mke wa tatu lakini hakuwa bomba kama second wife na sijuhi alimtoa wapi (labda kijijini wasikomjua)


Naogopa sana wanaume/wanawake wanaofiwa more than once. Hata kama ni wazima wanaweza kuwa na nuksi au ushirikina kwenye ukoo.


wa kwanza et alikufa kwa ugonjwa wa ini, wa pili cancer
 
Nyumba Kubwa amesema nilichotaka kusema. Kuna swala la ushirikina, lisiwe ignored hata kama mmepima na kukuta mambo safi. Au ana lispiritual wife ambalo huuwa wake wa kibinadamu, kufiwa wake 2 yatia shaka.

Maisha ni zaidi ya ndoa, na God's time is the right one. Asubiri na hata asipoolewa bado haimfanyi kuwa nusu binadamu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…