Shukrani sana 'Bonge' wa Clouds FM

Shukrani sana 'Bonge' wa Clouds FM

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,307
Reaction score
25,932
Hivi karibuni, humuhumu JF, niliandika kwa kuuliza: Kwanini mabasi ya mikoani 'yalazimishwe' kuingia kila stendi?.

Leo, asubuhi katika kipindi cha Power Breakfast, mtangazaji 'Bonge' alikuwa na mazungumzo na wadau wa usafirishaji kwa mabasi makubwa.

Hakika, wadau wanalalamikia kitendo cha mabasi ya mikoani kulazimishwa kuingia na kutoka kwenye kila stendi zilizopo wanapopitia.

Natoa shukrani zangu za dhati (awe alisoma humu au la) kwa Mtangazaji 'Bonge' kwa kuiongezea hoja yangu kwa jamii.

Ipo haja ya suala hili kutazamwa na kufanyiwa kazi kwa mustakabali mwema wa taifa letu
 
Wengine huwa wanatoa tu posho wanapita juu kwa juu..
 
Mnalazimishwa kuingia ili mlipe ushuru, although kuna wakati inafanyika vile ili bus likisimama angalau abilia waache shs mbili tatu kwa kununua chochote eneo hilo.

But kwingine ni mateso sana, basi linaelekea bukoba, musoma hama kigoma huko, yaani pale gairo, bagamoyo au nzega hakuna abilia wa kupanda au kushuka mnaambiwa 'arooo ingia kure' ,,😆
 
Hili jambo lina hasara nyingi kuliko faida kama wakiruhusu mabus kutoingia stand,Kwanza madereva na makondakta wataanza waambia wateja (stend flani hatuingiii) abiria kashazoea kupanda bus flan leo hii konda na dereva wanaleta utaratbu wo. (kero kwa abiria)

Pia kuna abiria wanaopandia njiani,bus lispoingia stand itapelekea abiria wasubiri mabus kwenda kujipanga Barabarani ili kujaribu kusimamisha magari maana nina uhakika hili likiptishwa ni mabus machache sana yatakua yanaingia stand,mengi yatakua yananyoosha goti,hii itapelekea shida ya usafiri kwa abiria wa Njiani.

Ajali zitaongezeka kwasababu machinga wote waliokua stand wengi watakua kule barabaran wakisubiri mabus yapite maana huku stand mabus yatakua hayaingii na yakiingia n moja moja tu,so machinga wataptiwa sna na mabus wakiwa wanauza vitu madrishani.

Bus kuingia stand hata kama halisimami kitendo cha kuingia tu linaacha Ushuru,kusaidia uendeshwaji wa stand husika lkn pia linatoa fursa kwa wateja wahtaji vocha na vtu vdg dogo ambavyo havipatkan ndani ya gari.

Ki ufupi hili swala wala sio la kulitetea au kulipgia kelele hizo stand ni za mabus na zilijengwa kwa ajili ya mabus na abiria,BUS kuingia stand ni Lazima na sio Ombi kwa usalama wa Wananchi,Kwa maendeleo ya Taifa,nk
 
Niliunga mkono mada yako kwa sababu mimi ni mdau wa kusafiri na haya ma bus na kiukweli abiria wengi ukiacha wamiliki wa busses hulalamikia sana huu upuuzi... Kero nyingine ni ile hoja ya kipuuzi kabisa ya kuzuia mabus yasisafiri usiku kwa kisingizio cha usalama wakati nchi ina vyombo kibao vya ulinzi na usalama. Bus inatoka Kigoma, Katavi, Mbeya etc zinaingia Dar usiku wa manane, kwa nini bus isisafiri usiku na kuingia Dar na kwingineko saa 12 asubuhi?
 
Hili jambo lina hasara nyingi kuliko faida kama wakiruhusu mabus kutoingia stand,Kwanza madereva na makondakta wataanza waambia wateja (stend flani hatuingiii) abiria kashazoea kupanda bus flan leo hii konda na dereva wanaleta utaratbu wo. (kero kwa abiria)

Pia kuna abiria wanaopandia njiani,bus lispoingia stand itapelekea abiria wasubiri mabus kwenda kujipanga Barabarani ili kujaribu kusimamisha magari maana nina uhakika hili likiptishwa ni mabus machache sana yatakua yanaingia stand,mengi yatakua yananyoosha goti,hii itapelekea shida ya usafiri kwa abiria wa Njiani.

Ajali zitaongezeka kwasababu machinga wote waliokua stand wengi watakua kule barabaran wakisubiri mabus yapite maana huku stand mabus yatakua hayaingii na yakiingia n moja moja tu,so machinga wataptiwa sna na mabus wakiwa wanauza vitu madrishani.

Bus kuingia stand hata kama halisimami kitendo cha kuingia tu linaacha Ushuru,kusaidia uendeshwaji wa stand husika lkn pia linatoa fursa kwa wateja wahtaji vocha na vtu vdg dogo ambavyo havipatkan ndani ya gari.

Ki ufupi hili swala wala sio la kulitetea au kulipgia kelele hizo stand ni za mabus na zilijengwa kwa ajili ya mabus na abiria,BUS kuingia stand ni Lazima na sio Ombi kwa usalama wa Wananchi,Kwa maendeleo ya Taifa,nk
Hoja dhaifu Sana... Kwanza usichojua ni kwamba haya makampuni ya mabus yana maajenti kwenye vituo mbalimbali na wana mawasiliano nao. Hivyo kama bus halijajaa wanawasiliana nao mapema na wataingia stend. Hivi nikuulize bus kama SAULI, IMAN, SHABIB na mengine imetoka Dar siti zote zimejaa inaingia KIBAHA stend kufanya nini hasa?? Pili kama bus halijajaa na linahitaji abiria lazima wataingia stend tuu, hoja iliyopo ni kuweka ulazima wa kuingia kila stend wakati tayari bus imejaa, what for??
 
Hivi karibuni, humuhumu JF, niliandika kwa kuuliza: Kwanini mabasi ya mikoani 'yalazimishwe' kuingia kila stendi?.

Leo, asubuhi katika kipindi cha Power Breakfast, mtangazaji 'Bonge' alikuwa na mazungumzo na wadau wa usafirishaji kwa mabasi makubwa.

Hakika, wadau wanalalamikia kitendo cha mabasi ya mikoani kulazimishwa kuingia na kutoka kwenye kila stendi zilizopo wanapopitia.

Natoa shukrani zangu za dhati (awe alisoma humu au la) kwa Mtangazaji 'Bonge' kwa kuiongezea hoja yangu kwa jamii.

Ipo haja ya suala hili kutazamwa na kufanyiwa kazi kwa mustakabali mwema wa taifa letu
RC wa Dar Amos Makalla ametimiza wajibu wake, Sasa ruksa mabasi kupakia abiria kwenye stendi binafsi.
 
Hapana nakataa kabisa hawajaruhusu,
Jana Nimekata Tiketi Shekilango Allys Bus,
Wamesema Abiria wooote wanatakiwa Kupandia Mbezi stand ya Magufuli huo ndio Muongozo na Hakuna Kupakia Pengine Kama Ilivyokuwa awali,Mwanzo tulikuwa tunapandia Shekilango.Dar-Mwanza.
 
Back
Top Bottom