Pre GE2025 Shukrani ziwaendelee wote waliowezesha na kufanikisha Wiki ya Maandamano, Kishindo chake kimetikisa nchi

Pre GE2025 Shukrani ziwaendelee wote waliowezesha na kufanikisha Wiki ya Maandamano, Kishindo chake kimetikisa nchi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Kwa niaba ya Waandaaji wa wiki ya Maandamano ya Amani (awamu ya kwanza) na kwa niaba ya Wapenda haki wote duniani, nachukua Fursa hii kuwashukuru watu wote kutoka pande waliowezesha Maandamano hayo kufanikiwa na kutikisa kwa kishindo, ambapo imedhihirika sasa kwamba yameacha gumzo Duniani kote.

Screenshot_2024-04-30-23-53-42-1.png
Screenshot_2024-04-30-19-29-27-1.png


Shukrani ziwafikie wote kabisa waliosambaza taarifa za Maandamano hayo kote duniani, tunaishukuru sana JF kwa kuruhusu taarifa za Maandanano hayo kuwemo humu 24/7 bila kikwazo chochote, pamoja na vurugu za wahafidhina za kuchomekea lugha chafu ili kutukatisha tamaa, kwa kweli tutakuwa wachoyo wa fadhila ikiwa tutashindwa kumshukuru Waziri wa Habari Mh Nape Nnauye, ambaye alitumia muda wake vizuri kusambaza taarifa za Maandamano hayo ndani ya Bunge la Tanzania, tena aliyasambaza kwa weledi na kwa usahihi kabisa.

Bali hatuna cha kuwalipa wale waliowezesha Maandamano hayo kwa hali na mali, kwa dua na maombi, kwa pesa na michango yao yote waliojitolea, Tunamuomba Mwenyezi Mungu awarudishie ukarimu wao mara nyingi zaidi ya walichotoa, Kazi waliyoichangia ni kazi ya Mungu mwenyewe kabisa na ndio maana mnaona Kishindo cha Tanganyika

Mungu ibariki Chadema, Mungu Ibariki Tanganyika
 
Wadudu Arusha oyeee

Tundu Antipas Lisu anatisha sana

Kanisa Moja Takatifu la Mitume 😂😂😂
 
Labda kama kimetisha familia zenu, mtaani Chadema hamskiki kabisa.
 
Kiukweli ishu ya muungano na utanganyika nilikuwa siichukulia kwa uzito kiivyo, lkn sasa hivi nimebadili mtazamo hata huku mtaani nipoishi gumzo ni hilo hilo.
 
Kiukweli ishu ya muungano na utanganyika nilikuwa siichukulia kwa uzito kiivyo, lkn sasa hivi nimebadili mtazamo hata huku mtaani nipoishi gumzo ni hilo hilo.
Hayo ni mafanikio ya Maandamano
 
Back
Top Bottom