Shukuru kawambwa popote ulipo naomba usikie kilio cha wanafunzi waliorejeshwa masomoni udom.

Shukuru kawambwa popote ulipo naomba usikie kilio cha wanafunzi waliorejeshwa masomoni udom.

REAL ACTIVIST

Member
Joined
Dec 2, 2012
Posts
39
Reaction score
5
Mheshimiwa waziri wa elimu Dk.Shukuru Kawambwa naomba utambue tu kuwa jamii yote ya watanzania wakiwemo wasomi kama wewe inafahamu kuwa wewe ndiye waziri mwenye dhamana ya kuhakikisha gurudumu la maendeleo katika sekta ya elimu hapa Tanzania linazunguruka na kato huwezi kuliacha likalegalega na mwishowe likasimama.Sasa basi kama hivyo ndivyo,nadhani mheshimiwa waziri hutawaacha wanafunzi wa UDOM waliokuwa wamesimamishwa masomo na sasa wamerejeshwa masomoni aidha wafe njaa au mwisho wa siku wajepata shahada zenye viwango vya kuchechemea kwasababu ya kutopewa pesa za kujikimu kwa wakati muafaka kwa kufuata mujibu wa sheria na talatibu zilizoainishwa kwenye sera ya serikali ya elimu ya juu.Mheshimiwa waziri wa elimu,naamini hakuna usichokifahamu kuhusiana na wanafunzi hawa wa UDOM ambao wamerejeshwa masomoni baada ya kusimamishwa taangia mwaka wa jana.Mheshimiwa waziri wa elimu naomba ulitazame suala la wanafunzi hawa kwa upana na urefu ili kuwanusuru na maisha magumu wanayokumbana nayo kwa sasa kwani hawajapewa pesa za kujikimu taangia mwezi wa oktoba mpaka sasa.kwakuwa mheshimiwa waziri ni mwajibikaji katika wizara yako naamini utasikia hiki kilio cha hawa wanafunzi wahanga wa UDOM,Mungu ibariki UDOM,Mungu ibariki Tanzania Ameeeen.Naomba kuwasilisha.
 
Tukumbuke pia wanafunzi wa SUA,Kwani toka oktoba hatujapata pesa ya kujikim.Verification tulishafanya lakini bodi haijatupa pesa kwa miezi miwili sasa licha ya kuahidi kutupa mapema tu pesa hizo.Ndugu waziri tunaish maisha magum sana kwan wengi tu watoto wa wakulima,kiujumla hatuna aman kabisa na maisha ya chuo.Tunaomba sana utunusuru na hii hali
 
Poleni jombaa mnanikumbusha nyakati za kukomnika,
njaa ikiuma module hazipandi,
unapita kila room ukipata hata mkate unapiga bila hata kukaribishwa,

lakini pianahisi mnapaswa kufikisha malalamiko sehemu husika kwa barua rasmi na sio mitandaoni ndugu zangu, kama serikali ya wanaafunzi haina ushirikiano undeni ushirikiano kwa :attention🙁amani elezeni) matatizo yenu kwa kufata taratibu....

Tumieni wabunge fulani fulani kama njia mbadala kufatilia ishu yenu (it works nanyi mwajua, na mwawajua wale wanaosaidia vitu hivi..mambo mengine pia siasa ni muhim kwani utoa msukumo) maana wale bodi huwa hawajua njaa na serikali yao (mpaka wapate misukumo)
 
Hivi nani mnayemwita mwajibikaji? Moja kati ya majitu bomu ambayo hayakutakiwa kunusa kwenye magari yanayoendeshwa kwa kodi zetu ni huyu. Mmesahau alivyoiacha tanroads mpaka mrema akajenga utawala wake wa kugawa tenda kwa birders wenye gharama kubwa zaidi na ye kuchukua cha juu kabla hata tenda haijatolewa?
 
Back
Top Bottom