Shule kuwaondoa wanafunzi wenye alama za chini

LUS0MYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 4, 2011
Posts
866
Reaction score
1,109
Wadau tujadili hizi shule hasa binafsi kuweka alama za wastani ambazo kama mwanafunzi asipofikishwa anatakiwa kurudia darasa au kuondolewa shule.

Hii inasababishwa na hali ya shule kuondoa wanafunzi wenye uelewa mdogo ili kufanya shule kupata sifa ya ufaulu..je hii ni halali?na kama mzazi akilazimisha mtoto aendelee na shule,uongozi wa shule unaweza kumkatalia?na kama wakimkatalia mzazi anaweza kuchukua hatua gani za kiwizara au kisheria....hii hali imezidi sana inabidi ikomeshwe.
 
Kama hayamwingii anayofundishwa kwanini apelekwe mbele? arudie mpaka aelewe anachofundishwa.
 
Kama hayamwingii anayofundishwa kwanini apelekwe mbele? arudie mpaka aelewe anachofundishwa.

Kosa la kulazimisha mambumbumbu kusonga mbele hata kama kichwani kuna kamasi ndiko kulikoiletea aibu shule ya Feza baada ya Mwanahasha peke yale kupata division Five wakati waliobaki wote wana division One na Two tu.

Hili la kurudisha Mambumbumbu darasa linaongeza uwajibikaji kwa mwanafunzi na mzazi. Ndiyo siri ya ufauru wa seminary schools.
Umeelewa?
 
serikali kupitia kamishina mkuu wa elimu imetoa waraka mwaka huu ukipinga jambo hili. baadhi ya shule ilifikia hatua ya kubambikiza makosa kwa wanafunzi wanaohisi hawatafaulu na kuwafukuza shule.

Kwa mujibu wa waraka huo, ni makosa kwa shule kuwaondoa wanafunzi walio katika mwaka wa mtihani bila ushiriki wa AFSA ELIMU MKOA (ambaye kisheria ni mjumbe wa bodi zote za elimu).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…