Nelson Masaduki
JF-Expert Member
- Oct 27, 2017
- 346
- 380
Watanzania wenzangu,
Nimefurahishwa na wazo lililotolewa Bukoba kuwa, itaanzishwa shule maalum ili kumuenzi Ruge Mutahaba. Tangu alipopumzishwa ndugu yetu Ruge Mutahaba, watu wengi wametoa yaliyomo mioyoni mwao na kuthibitisha kuwa, licha ya Ruge kuwa ni mtu wa kawaida katika masuala ya sanaa, burudani na tasnia ya habari - Kijana huyo alikuwa ni kiungo mzuri katika kuwasaidia vijana kuziona fursa. Fursa ni moja ya maneno ambayo aliyatumia vizuri katika kuwajengea uwezo vijana kuona namna wanavyoweza kupata fedha ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Nadhani hatua hiyo ni ya kuungwa mkono na juhudi za Maprofesa walioko Bukoba zitasaidia kuiweka taasisi hiyo katika ubora unaotakiwa. Mungu ibariki Tanzania,
Nelson,
Geita
Nimefurahishwa na wazo lililotolewa Bukoba kuwa, itaanzishwa shule maalum ili kumuenzi Ruge Mutahaba. Tangu alipopumzishwa ndugu yetu Ruge Mutahaba, watu wengi wametoa yaliyomo mioyoni mwao na kuthibitisha kuwa, licha ya Ruge kuwa ni mtu wa kawaida katika masuala ya sanaa, burudani na tasnia ya habari - Kijana huyo alikuwa ni kiungo mzuri katika kuwasaidia vijana kuziona fursa. Fursa ni moja ya maneno ambayo aliyatumia vizuri katika kuwajengea uwezo vijana kuona namna wanavyoweza kupata fedha ili waweze kujikwamua kiuchumi.
Nadhani hatua hiyo ni ya kuungwa mkono na juhudi za Maprofesa walioko Bukoba zitasaidia kuiweka taasisi hiyo katika ubora unaotakiwa. Mungu ibariki Tanzania,
Nelson,
Geita