KERO Shule ya Msingi na Sekondari Goba Mpakani zinawarudisha nyumbani na kuwachapa wanafunzi wasio na hela ya chakula

KERO Shule ya Msingi na Sekondari Goba Mpakani zinawarudisha nyumbani na kuwachapa wanafunzi wasio na hela ya chakula

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mimi ni Mdau wa Elimu ninayeishi Goba Mpakani, Mtaa wa Tegeta A, Kata ya Goba, kuna changamoto ambayo imejitokeza ni miezi kadhaa sasa inaendelea kuwa kikwazo kwa Watoto wa Shule kupata haki yao ya msingi ya kupata elimu bora.

Kuna utaratibu ambao umeanzishwa na Uongozi wa Shule ya Msingi Goba Mpakani pamoja na Shule ya Sekondari Goba Mpakani.

Shule hizi zote ni za kutwa na zinapatikana eneo la Goba Mpakani, zipo karibu sana na zinatazamana, utaratibu ulioanzishwa ni kwamba kila siku Mwanafunzi anapeleka Shuleni Shilingi 1,000, kwa ajili ya kupikiwa chakula cha mchana hapo shuleni, ambapo wanapikiwa Wali Maharage.

Sasa changamoto inayojitokeza si kila Mzazi anaweza kumudu gharama hizo kwa kila siku kumpatia mtoto wake Shilingi 1,000 na ikizingatiwa unakuta mzazi mmoja ana watoto wawili au mpaka Watatu wengine wanasoma Shule ya Msingi na mwingine anaweza akawa anasoma Sekondari.

Uongozi wa Shule unachofanya kama Mwanafunzi amekosa Shilingi 1,000 anachapwa viboko na anatakiwa kurudi nyumbani hadi atakapokuja na hela.

Hivyo, Watoto wamekuwa hawaendi shule na wanakosa vipindi sababu ya kukosa 1,000 ya kula Wali Maharage.

Uongozi wa Shule umefanya kuwa mchango wa hela ni lazima na sio ombi, bila kuangalia ni kwa kiasi gani Wanafunzi wengi wanapata athari kitaaluma kwa kushindwa kuhudhuria vipindi vya darasani kwasababu kakosa buku ya chakula.

Hili jambo kama Mdau wa Elimu naliona linadhorotesha sana juhudi zinazofanywa na Serikali Kuu kuhakikisha kila Mwanafunzi au Mtanzania anapata elimu bure na bora kwa haki bila kujali hali ya uchumi wake.

Naomba hili suala likemewe, kwa Wazazi watakaoshindwa ku-afford hizo hela Watoto wao wapate fursa sawa ya kusoma kama ilivyo kwa wengine na sio kufukuzwa kurudi nyumbani ilhali masomo yanaendelea.

Pia soma: Mchengerwa: Wanafunzi wote wa kutwa wapate chakula shuleni
 
Kwakweli serikali inatakiwa kuliangalia hili sio sawa kabsa,mzazi anawazaatoe nauli lkn hapo hapo na hela ya chakula? Kwann mwanafunzi asiachwe kama Hana hela kuliko kumfukuza? Mamlaka husika zifuatilie kwakweli!.
 
Mtoto wako akikaa nyumbani Msosi wa Buku humpi? Mtoto akila shuleni, msosi wa buku kuna shida gani. Watoto mnawaachia asubuhi hujampatia hata chai, arudi kula saa 2 usiku mpaka saa 2 usiku kesho? Acheni hizo, tafuteni hizo buku muwape. Hela wengine wanazo, wanasingizia Elimu Bure.
 
Bado adui wa taifa UJINGA anasababisha maskini azidi kuwa maskini. Hao wazazi wanaolalamikia watoto kula shuleni ni maskini waliojaa upumbavu na ujinga uliotukuka. Mtoto asiyepata lishe atawezaje kuwa bora baadae? Au wazazi hawajui kuwa kwenye usaili mwonekano pia ni kigezo muhimu kisichotajwa? Mtoto anayepata lishe duni ataonekana mzee kabla ya muda wake.

Tutaendelea kutawaliwa na watoto wa viongozi kwa sababu wao husomesha watoto shule nzuri na huhakikisha hawakimbii majukumu yao. Maskini atazidi kuwa maskini. Katika kitu kimesaidia wachaga kuwa bora sana ni kuhakikisha watoto kuanzia msingi wanakula shuleni. Nilisoma darasa la kwanza hadi la 3 shule ya msingi Lambo, Machame nakumbuka tulikuwa tunakula shuleni.
 
Mimi ni Mdau wa Elimu ninayeishi Goba Mpakani, Mtaa wa Tegeta A, Kata ya Goba, kuna changamoto ambayo imejitokeza ni miezi kadhaa sasa inaendelea kuwa kikwazo kwa Watoto wa Shule kupata haki yao ya msingi ya kupata elimu bora.

Kuna utaratibu ambao umeanzishwa na Uongozi wa Shule ya Msingi Goba Mpakani pamoja na Shule ya Sekondari Goba Mpakani.

Shule hizi zote ni za kutwa na zinapatikana eneo la Goba Mpakani, zipo karibu sana na zinatazamana, utaratibu ulioanzishwa ni kwamba kila siku Mwanafunzi anapeleka Shuleni Shilingi 1,000, kwa ajili ya kupikiwa chakula cha mchana hapo shuleni, ambapo wanapikiwa Wali Maharage.

Sasa changamoto inayojitokeza si kila Mzazi anaweza kumudu gharama hizo kwa kila siku kumpatia mtoto wake Shilingi 1,000 na ikizingatiwa unakuta mzazi mmoja ana watoto wawili au mpaka Watatu wengine wanasoma Shule ya Msingi na mwingine anaweza akawa anasoma Sekondari.

Uongozi wa Shule unachofanya kama Mwanafunzi amekosa Shilingi 1,000 anachapwa viboko na anatakiwa kurudi nyumbani hadi atakapokuja na hela.

Hivyo, Watoto wamekuwa hawaendi shule na wanakosa vipindi sababu ya kukosa 1,000 ya kula Wali Maharage.

Uongozi wa Shule umefanya kuwa mchango wa hela ni lazima na sio ombi, bila kuangalia ni kwa kiasi gani Wanafunzi wengi wanapata athari kitaaluma kwa kushindwa kuhudhuria vipindi vya darasani kwasababu kakosa buku ya chakula.

Hili jambo kama Mdau wa Elimu naliona linadhorotesha sana juhudi zinazofanywa na Serikali Kuu kuhakikisha kila Mwanafunzi au Mtanzania anapata elimu bure na bora kwa haki bila kujali hali ya uchumi wake.

Naomba hili suala likemewe, kwa Wazazi watakaoshindwa ku-afford hizo hela Watoto wao wapate fursa sawa ya kusoma kama ilivyo kwa wengine na sio kufukuzwa kurudi nyumbani ilhali masomo yanaendelea.
Serikali inataka wanafunzi wale shuleni, hao wazazi wapambane
 
Mimi ambacho najiuliza mpaka sasa walimu kumchapa mtoto kisa hana hela ya kutoa kwa kitu kinachotakiwa shuleni huwa inamaanisha nini hapo ninapo shindwa kuelewa
 
Back
Top Bottom