A
Anonymous
Guest
Kama inavyoonekana hapo ndani haikidhi kabisa kwa matumizi ya Wanafunzi kwa kuwa majengo yake si rafiki na yanahatarisha usalama wa watumiaji wengi wao wakiwa ni Wanafunzi na Walimu.
Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ameshaandika barua sehemu tofauti kwa ajili ya changamoto iliyopo katika majengo ya shule hiyo lakini hakuna hatua ambazo zimechukuliwa.
Shule hiyo ina miradi inayojitegemea ikiwemo ya Mikorosho ambayo inawawezesha kupata fedha lakini pesa za matumizi ya Shule hazijulikani zinapokwenda, Mtendaji Kata amekuwa changamoto ya fedha kutoonekana na hazijulikani zinaenda wapi.
Shule hii ipo katika Jimbo la Mbunge na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Hamis Ulega.
Kinachoendelea ni aibu kwa kweli, tazaman video hizi zinazoonesha maisha wanayopitia Wanataaluma wa shule hii, angalia ukuta, nyufa, vyoo na madarasa yalivyo.