Shule ya msingi yaweka rekodi ya kutofelisha hata mwanafunzi mmoja kwa miaka 10

Shule ya msingi yaweka rekodi ya kutofelisha hata mwanafunzi mmoja kwa miaka 10

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Untitled-1_3.jpg
Shule ya Msingi Laalakir iliyopo Kijiji cha Partimbo, Kata ya Partimbo wilayani Kiteto Mkoani Manyara, imekuwa na matokeo ya alama "A" kwa miaka 10 mfululizo na kushika nafasi ya kwanza kiwilaya na kimkoa na haijawahi kufelisha mwanafunzi

Wanafunzi waliofanya mtihani mwaka 2022 ni 36, kati ya hao 35 wamepata alama A na B mmoja.

Shule hii ilijengwa na watu wa Jamhuri ya China kati ya shule tatu zilizojengwa, Tanzania Bara na Visiwani, moja ilijengwa Kiteto Manyara, nyingine Mkoa wa Pwani na moja Zanzibar.


Chanzo: EATV
 
Kwa hiyo idadi ungefelisha? Yaani 36! Sasa hapa kwetu Kuna shule private haijawahi kutoa B ni mwendo wa A tu. Lakini za serikali Kuna shule ilikua na wanafunzi 233 wamefeli 27. Idadi ya wanafunzi darasani inaathiri matokeo.
 
Back
Top Bottom