Shule ya sheria (law school)

MAKINYA

Senior Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
139
Reaction score
54
Idadi ya watanzania wanaohitaji hudma ya mawakili inazidi kuongezeka hasa maeneo ya vijijini ambako mawakili wachache waliopo hawapendi kufanya kazi mana wengi wamejikita dar na maeneo mengine ya mijini.
Changamoto ninayoiona kuchangia uhaba huu wa mawakili pamoja na gharama za ada kuwa kubwa,lakini kubwa zaidi ni hili la kuendeshea mafunzo sehemu moja tu ya nchi,ni bora basi mafunzo haya yakaendeshwa katika kanda yaani nyanda za juu kusini kuwa na kituo kanda ya kati na kanda ya kasikazini,hii ingepunguza gharama kwa watu wengi na huku ikizalisha mawakili wengi.
 
Kumbuka kuwa muundo wa mahakama ni Mahakama ya rufaa kama mahakama ya juu kabisa, hii ipo Dar es Salaam, ingawa hufanya vikao vyake kwenye kanda za mahakama kuu. Mahakama kuu, sharia imegawa mahakama kuu kwenye kanda, kwa sasa karibu kila mkoa ni kanda ya mahakama kuu isipokuwa mikoa ya shinyanga, kigoma, pwani, morogoro,Singida,Lindi, Mara na Manyara ( utanisamehe mikoa mipya siifahamu). mahakama ya hakimu mkazi ambazo zipo kila mkoa na mahakama ya wilaya, ambazo zipo kila wilaya ( mahakama ya wilaya na hakimu mkazi zina karibu mamlaka sawa, na chini kabisa kuna mahakama za mwanzo. Mahakama za mwanzo ndizo nyingi sana na ziko vijijini. Kwa muundo huu utaona kuwa mahakama ya mwanzo inahudumia wananchi wengi kutokana na ukweli kuwa ni mahakama ya chini na imetapakaa karibu kila mahali. Sheria hairuhusu mawakili kufanya uwakilishi kwenye mahakama za mwanzo na kwa sababu hiyo mawakili kisheria hawawezi na hawatakiwi, kisheria kuhudumu kwenye mahakama hizo.Gharama sio tatizo kwani kuna mashirika mengi yanayayotoa msaada wa bure wa kisheria kama vile NOLA, kituo cha sheria na haki za Binadamu, Chama cha wanasheria wanawake TAWLA, WILDAF na kadhalika. Sambamba na hivyo kuna paralegals ambao ni wanasheria ambao sio mawakili na wao wanajikita kutoa msaada wa kisheria bure kwa wahitaji wa huduma hiyo. Kwa misingi hiyo sioni kama kuwa na kanda za shule ya sharia ni suluhisho la tatizo.
 
Wasomaji samahani mashine ninayotumia imegoma kushirikiana name haiweki paragraphs, Nadhani nitaeleweka pamoja na mapungufu
 
Pamoja na shule kuwa moja tu, ila bado limekuwepo tatizo la wanaf. Weng kushindwa kuhitimu kutokana na kufeli mitihan.
 

Tumekuelewa usijali mpendwa, but kupanua wigo kwa upande wa law xul, kutaathiri nini mahakama za Tanzania? sana sana nikionacho mie, kutapunguza usumbufu fulani unaojitokeza. Mfano, vyuo vingapi vinavotoa mafunzo ya sheria? jibu ni kuwa kuna vyuo vingi na vilivotapakaa mikoa tofauti. Watu waishio mikoani wanasaidiwa vipi kutimiza malengo yao kwa kujiunga na law xul?
Ni dhairi kuwa, nchi yetu ni masikini sana na bado inahitaji wasomi wengi zaidi na sio misaada mingi zaidi. Law School tuliyonayo, inakidhi vipi mahitaji ya walio wengi?
Tunasoma tu ili iwe BORA KUAPISHWA?
Kutokana na wingi wa wahitaji, njia gani bora inatumika kuhakikisha inatoa advocate wanaofahaa ukiachilia mbali mitihani. Binafsi huwa nina amini, kuna zaidi ya kufanya mtihani katika kupima akili ya mtu.
Je njia hizo zinakidhi uwepo wa wanafunzi wote waliojiunga?
Hayo ni mawazo tu.
 
NG, Ukiangalia setup ya mahakama ilivyo hapo juu unapata scenario ifuatayo, mahakama za mwanzo ambazo ndio nyingi na ziahudumia idadi kubwa ya wananchi mawakili hawaruhusiwi kutetea. Lakini Magistrates Court inaruhusu rafiki na au ndugu ( see section 33) in this case a paralegal can appear. Wahitaji wengi wa sheria wako vijijini na mijini pia wahitaji wa sheria wameconcetrate kwenye sehemeu zenye hela on kwa mfano Mkoa wa Mbeya mawakili wote wamejazana jiji la mbeya na kuacha wilaya zake zote Rungwe, Chunya, Mbozi, Momba, Ileje, Mbalari bila mawakili. Anagalia Dar es salaam wilaya ya Ilala inaongoza kwa wingi wa mawakili ikifuatiwa na Kinondoni halafu Temeke. ukiangalia sababu utakuta mawakili wengi hupenda kuwa based kwenye RMS courts na High Court. Kwa hiyo hata tukiendelea kuweka zones kwa ajili ya Law school, target client yao itakuwa ni District Courts Resident Magistrates Courts na High Court na wale wa primary court watabakia bila uwakilishi,.
 

Pamoja na hayo yote bado nahao mwakili waliomijini hawajitoshelezi, mwakili wengi hawajaspecialize kwenye specific branch ya law hii ni kwa sababu wahitimu wengi wanafocus kufahuru law school tu maana ndio kikwazo kikubwa cha kupata mawakili, ni imekua point ya kudisappoint wanasheria wengi wene nia nzuri ya kutaka kuwa mawakili. Achilia mbali gharama za kumudu masomo hayo
 
There are two things here, one inadequacy of advocates ( not sure if your rating whether its on quantity or quality), secondly is the issue of specialization. As you are aware legal service is for sale the best lawyers are usually the most expensive, its like that all over the world, so if you want a good lawyer and you cant hire him because you do not have sufficient resources then you cannot say that we lack advocates. I would agree if you could have said there no access to justice. lawyers can specialize but watch out if that happens legal service will be more expensive very expensive as a lawyer will need only few cases in a year to make him survive, so he will make sure that he charges in such a way that he is comfortable the whole year.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…