Baba_Enock
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 7,076
- 2,457
Wakati Baba_Enock akisoma Shule ya Msingi Rumuli/Kashasha na Shule ya Sekondari ya Ufundi Moshi/Sengerema, asubuhi kabla ya kuanza masomo kulikuwa na utaratibu wa kukusanyika wanafunzi wote na kuimba "Wimbo Wa Shule". Siku za hivi karibuni naona huu utaratibu umetoweka katika shule za msingi na sekondari. Wanafunzi wanaingia madarasani kama "ngombe wanaingia zizini"!
Inawezekana kuwa ni maendeleo, lakini hizi "nyimbo za shule" zilikuwa zinaleta sana hamasa kwa wanafunzi kuwa "watiifu" na "wawajibikaji" na pia "kuweka bidii katika masomo"!
Kwa mfano (Shule ya Sekondari ya Ufundi Moshi" tuliimba hivi:
Shule yetu Ufundi Mungu Ibariki,
Bariki wanafunzi nao Walimu,
Tupate Amani, Upendo, Umoja,
Ushirikiano nao udumu daima,
Kiitikio
Tuwe watu watii,
Tuwajibike,
Na Kuzibuni Mbinu za Kazi daima X 2
Heshima ni muhimu kwa jumuiya,
Katika kuzibuni mbinu za kazi,
e.t.c
Skulimeti wangu Asprin anaweza kunishahihisha na kuongeza beti ya pili!
Swali: Kwanini Wizara imeamua kuua huu utaratibu?
Nawatakie Mapumziko mema ya mwisho wa mwaka na sikukuu njema ya Noeli
Inawezekana kuwa ni maendeleo, lakini hizi "nyimbo za shule" zilikuwa zinaleta sana hamasa kwa wanafunzi kuwa "watiifu" na "wawajibikaji" na pia "kuweka bidii katika masomo"!
Kwa mfano (Shule ya Sekondari ya Ufundi Moshi" tuliimba hivi:
Shule yetu Ufundi Mungu Ibariki,
Bariki wanafunzi nao Walimu,
Tupate Amani, Upendo, Umoja,
Ushirikiano nao udumu daima,
Kiitikio
Tuwe watu watii,
Tuwajibike,
Na Kuzibuni Mbinu za Kazi daima X 2
Heshima ni muhimu kwa jumuiya,
Katika kuzibuni mbinu za kazi,
e.t.c
Skulimeti wangu Asprin anaweza kunishahihisha na kuongeza beti ya pili!
Swali: Kwanini Wizara imeamua kuua huu utaratibu?
Nawatakie Mapumziko mema ya mwisho wa mwaka na sikukuu njema ya Noeli
Last edited by a moderator: