Si akili kujisifia wala kukejeli kwa sababu ya maumbile ya asili

Si akili kujisifia wala kukejeli kwa sababu ya maumbile ya asili

GoldDhahabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2023
Posts
7,189
Reaction score
10,375
Naamini sitamkasirisha mtu kwa maoni yangu! Hivi ndivyo niaminivyo.

Uwe ni mweusi sana au mweupe mno ( japo inasemekana hakuna mtu mweusi wala mweupe)!

Uwe mfupi mno au mrefu kuliko kawaida!

Uwe na miguu mirefu au ngozi inayong'aa hata bila mafuta!

Vyo yote vile! Maadam hukuchangia chochote kuwa hivyo, haifai kujisifia. Labda umshukuru Mungu! Naam, afanyaye hivyo ana akili njema.

Maumbile ya mtu ni "ascribed status" na si "achieved status '. Maadam hana mchango alioutoa kuwa hivyo, hastahili kujisifia wala si haki kukejeliwa na mtu yeyote yule. Ukiona mtu anamkejeli kwa sababu ya mwonekano wake wa kuzaliwa ujue ana shida katika kufikiri kwake!

Alau kwa aliyejijengea uwezo wa kunyanyua vitu vizito kwa sababu ya mazoezi makali anaweza akajisifia. Kafikia hapo kwa juhudi zake. Ni achieved status!

Inasikitisha kuona baadhi ya watu wakijisumbua kurekebisha maumbile yao, si kwa sababu za kiafya, bali ili tu aonekane anavutia!

Wengine, hasa mabinti, wamejidunga sindano ili wawe na makalio makubwa! Kuna waliofanya makubwa zaidi ya hayo. Wapo wa kiume na wa kike.

Lakini yote hayo ni kwa sababu ya kutokujikibali! Kwa aliyejikubali, hata kama maumbile yake hayaonekani kama ni ya kawaida, ataheshimika tu!

Nilisoma mitandaoni kipindi fulani kuwa binti mmoja kutoka Sudan, nafikiri, ambaye alikuwa mweusi sana, alipofika Marekani, mwonekano wake huo uligeuka kuwa fursa kwake! Sikumbuki vizuri, lakini nafikiri alipata kazi inayoendana na uanamitindo hivi! Inawezekana kwa Waafrika wenzake alionekana kituko, lakini kwa sababu alikuwa amejikubali hakukimbilia mikorogo kujikoboa sura yake awe kama Mzungu. Alijikubali, hivyo na watu wengine waliishia kumkubali na kumtunuku!

Nigeria kulikuwa na wachekeshaji maarufu: AKI NA UKWA ( sijui wako wapi kwa sasa). Inawezekana kule kuwa wafupi sana ndiyo kulichochea wao kuwa maarufu sana duniani, mpaka nikaweza kuwafahamu.

Nick Vujicic kazaliwa hana miguu wala mikono! Lakini kwa kuwa amejikubali, kwa sasa anafanya jitihada kuwatia moyo watu wengine, wengi wao wakiwa ni watu waliozaliwa na viungo vyote kujikubali na kuyaishi maisha yao kikamilifu!

Usitafute kuishi kwa ajili ya kuwaridhisha watu wengine! Hsutaweza!

Mwenye akili hawezi kujivunia maumbile ya kuzaliwa nayo! Mwenye akili timamu hawezi kuwakejeli wengine kwa sababu ya upekee wa maumbile yao ya kuzaliwa!

Kitu anachoweza kufanya mwenye akili ni kumtukuza Mungu!

Jikubali ili ukubaliwe!
 
Nick Vujicic hana miguu wala mikono lakini kajikubali! Anaishi maisha ya furaha!

Anaheshimika ulimwenguni kote!

Ana mke mzuri!

Ana watoto wazuri!

Familia yake inamfurahia!

Ana hela!

Anasaidia wenye uhitaji!

Hayo yote yamewezekana kwa kuwa kajikubali!

Vinginevyo, angeishia kuwa ombaomba.
 

Attachments

  • NICK_VUJICIC_AND_THE_BEAUTIFUL_FAMILY__2024_(240p).mp4
    2.2 MB
Sasa kwamfano mimi ni andunje nijikubalije mzee
Mshukuru Mungu kwa kukutofautisha na wengine!

Jione wewe ni wa kipekee kwa ajili ya kufanya mambo ya kipekee ambayo watu wa kawaida hawawezi kufanya!

Ni faida na si hasara!
 
kuna status nlisoma hivi majuzi inasema, PUNGUZENI KUJIKUBALI MNATUCHEKESHA.. sasa sijui walikua wanamaanisha nini mleta uzi。
Sijui walichomaanisha, lakini nafahamu kuwa:
1. Usipojikubali hutaweza kuwakubali wengine!

2. Usipojikubali huwezi kuitumia kikamilifu uwezo uliojaliwa na Mungu!

3. Usipojikubali utaishia kuwa mtumwa wa wengine!
 
LEO JUMMA MUBARAK HAKIKA TWENDE MASJID TUOMBEE NDUGU ZETU WALIO KUFA NA WALIO KATIKA MATESO, NA WATU WOTE KWA UJUMLA. AMIIN
 
Sijui walichomaanisha, lakini nafahamu kuwa:
1. Usipojikubali hutaweza kuwakubali wengine!

2. Usipojikubali huwezi kuitumia kikamilifu uwezo uliojaliwa na Mungu!

3. Usipojikubali utaishia kuwa mtumwa wa wengine!
shukrani, ila hela inamchango kwenye kuongeza kujikubali。
 
shukrani, ila hela inamchango kwenye kuongeza kujikubali。
Siyo kweli mkuu!

Kuwa na hela bila kujikubali kutakufanya uzitumie vibaya ili ujioneshe ni wa "maana"

Kama hujajikubali, ukipata hela nyingi kunaweza kugeuka majanga kwako na kwa wengine!

Ni sawa na mtu asiyejikubali apewe madaraka makubwa! Walio chini yake watamkoma😀
 
Sasa kwamfano mimi ni andunje nijikubalije mzee
Jikubali aisee.Kuna faida kadhaa;-
1-Ni rahisi kuokota vitu vilivyodondoka au vilivyopo chini.
2-Ukila chakula au kupata kinywaji kinafika haraka tumboni na unashiba kwa muda mfupi.
3-Ukiwa unazurula usiku halafu ukakutana na askari wa doria ni rahisi kuwaambia wewe ni mtoto umetumwa dukani ununue mafuta ya taa.
4-Hutumii gharama kubwa kwenye mavazi.Unaweza kuchukua hata kaptula ya kaka yako ukavaa kama suruali.
5-Unalala hata juu ya stuli au ndani ya begi.Hauhitaji nafasi kubwa.
6-Mara zote utahurumiwa/sympathies na watu waki-assume ni kachalii fulani.
6-Utaachwa umalizie chakula kwa sababu unaonekana ni kadogoo.
7-Hata ukifikiria kinyumenyume utasamehewa kwa sababu ya umbo lako.
8-Unaweza kuamua kuwa mvivu tu.Hata mambo yako yahusuyo kesho yako utawauliza watu warefu.Wewe una relax tu.
 
Siyo kweli mkuu!

Kuwa na hela bila kujikubali kutakufanya uzitumie vibaya ili ujioneshe ni wa "maana"

Kama hujajikubali, ukipata hela nyingi kunaweza kugeuka majanga kwako na kwa wengine!

Ni sawa na mtu asiyejikubali apewe madaraka makubwa! Walio chini yake watamkoma😀
kuna siku utakuja kunielewa, tuombe uzima。
 
Screenshot_20240531-093154~2.jpg

Inafikirisha sana.
 
Nick Vujicic hana miguu wala mikono lakini kajikubali! Anaishi maisha ya furaha!

Anaheshimika ulimwenguni kote!

Ana mke mzuri!

Ana watoto wazuri!

Familia yake inamfurahia!

Ana hela!

Anasaidia wenye uhitaji!

Hayo yote yamewezekana kwa kuwa kajikubali!

Vinginevyo, angeishia kuwa ombaomba.
Alafu huyu jamaa ana watoto wanne nadhani. Nguvu zote za mikono na miguu zimehamia kwenye ule mguu wa kati atakuwa anashona cherehani balaa
 
Jikubali aisee.Kuna faida kadhaa;-
1-Ni rahisi kuokota vitu vilivyodondoka au vilivyopo chini.
2-Ukila chakula au kupata kinywaji kinafika haraka tumboni na unashiba kwa muda mfupi.
3-Ukiwa unazurula usiku halafu ukakutana na askari wa doria ni rahisi kuwaambia wewe ni mtoto umetumwa dukani ununue mafuta ya taa.
4-Hutumii gharama kubwa kwenye mavazi.Unaweza kuchukua hata kaptula ya kaka yako ukavaa kama suruali.
5-Unalala hata juu ya stuli au ndani ya begi.Hauhitaji nafasi kubwa.
6-Mara zote utahurumiwa/sympathies na watu waki-assume ni kachalii fulani.
6-Utaachwa umalizie chakula kwa sababu unaonekana ni kadogoo.
7-Hata ukifikiria kinyumenyume utasamehewa kwa sababu ya umbo lako.
8-Unaweza kuamua kuwa mvivu tu.Hata mambo yako yahusuyo kesho yako utawauliza watu warefu.Wewe una relax tu.
Najua vingine umeandika kwa utani!

Lakini ukweli ni kwamba kujikubali ndiyo hatua ya kwanza itakayokusaidia kuufaidi upekee wako.
 
Back
Top Bottom