Siamini naanza kuacha uhuni, umalaya, ubazazi na ubaradhuli. Huyu mtoto nimemuibua humu humu JamiiForums

Siamini naanza kuacha uhuni, umalaya, ubazazi na ubaradhuli. Huyu mtoto nimemuibua humu humu JamiiForums

GuDume

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2015
Posts
6,651
Reaction score
14,337
Waungwana habari za mchana. poleni na kazi ndugu zanguni. naandika hapa nikiwa nimefurikwa na furaha pomoni. katika harakati zangu za kutafuta mwenzi wa kufanana naye kwa mazuri naanza kuona uelekeo. waswahili wanasema "nyota njema huonekana asubuhi" na nimeamini "mwenda bure si sawa na mkaa bure" nimejipatia kimwana wa haja hasa.

siku nyingi nilikuwa natamani niweze kuibuka humu na mtoto mmoja mzuri classic anipende mimi na mauza uza yangu.awe mzuri wa sura,mwili na tabia isije ikawa story ile ya "uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti"

"jungu kuu halikosi ukoko" nimefanikiwa kumpata mtoto mmoja mzuri sana toka sehemu flani za tanganyika maarufu kwa kutoa mabinti warembo. nimegundua kumbe humu kuna mabinti hujitoa akili tu ila ukiwa nao nje wana akili nzuri zimetulia kabisa.amenishauri kuwa basi nipunguze ubazazi nami kuanzia leo nimeanza kubadilika. nitakuwa goodman kabisa...(ila tu siyo ndo watu wengine waanze kunitibua maana waswahili wanasema "jasiri haachi asili"

nawaambia ndugu zanguni" mgaa gaa na upwa hali wali mkavu" nami sasa nina anza kupata ahueni maana kumbukeni nliwahi kusema "mficha uchi hazai" nami nikaona kwa huyu dada nisifiche hisia zangu.(ingawa sisi wengine tushasahau kutongoza ) basi nikajiuma uma lakini maskini dada wa watu alishajua nia yangu ni nini... basi akanikubalia maana wahenga walisema "heri kenda nenda kuliko kumi nenda rudi" kanipata mkaka wa watu nlishafanya fanya uhuni kidogo nimetuliza majeshi.

nawashauri ndugu zangu.... nanyi mzidi kuwa na tabia njema ,wakweli na wawazi humu ndani watoto wazuri wapo sema ni mpaka uwe unajua kulenga... otherwise utaishia tu kunaniii....bint wa watu hana makuu. ana shughuli zake.ana mvuto na anajiamini sana.si mswahili maana mi nawaogopa sana wanawake wa uswahilini mkigombana mwanamke wa uswahilini anaweza akakusema vibaya mpaka ukafa.huyu hata kwa sauti yake ni ya utulivu haina papara na anajua kuzungumza lugha kuu mbili. english na swahili hivyo hatutakuwa na shida ya mawasiliano. siyo zile type za kunitumia smg... no si hizo.

nami nawaambia "ukuu kuu wa kamba si upya wa mkambaa, japo ni nyembamba na tena imechakaa" mlikuwa mnasema gudume wa nini.. mwenzenu mrembo kila siku alikuwa anasali atanipata lini.
 
ndugu zanguni (leo hata namna ya kuwa address imebadilika) nashukuruni sana kwa kweli... mtoto kaumbika... mashavu yake yote yanaonekana kuwa na mvuto,sura ya yai,lips za mfuto na macho ya goroli. rangi yake ya chungwa lilioiva ... akiongea ni kama hataki maana anaweka vituo vyote kwa usahihi kabisa. kwa kweli... "mla mla leo ,mla jana kala nini?" nami nimejipatia mtoto mantashallah... allahamdullilah "kimfaacho mtu chake" maana msije waswahili mkaanza kusema oohh.. sijui ni na nini... gudume amekutana na maneno ya wahenga ya kuwa "subra yavuta kheri"

ngoja nianze kulenga na mimi,hongera mkuu
Hongera sana
Hahahahhahahahahhaha
hata kama ni milioni?
Hongereni jaman nasubiria card ya mchango tu
Huyo ni Miss natafuta au Demiss hao chaote au mama wa huruma Jf...

Msinikoti please
Gudume siliamini
[emoji23]
Hongera sana huyoo bibie uliempata ni mwalimu wa kiswahili??
Hongera sana
 
Back
Top Bottom