Siasa Safi na Uongozi Bora: Sera hizi bado zipo?

Siasa Safi na Uongozi Bora: Sera hizi bado zipo?

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,207
Reaction score
13,839
1725620519525.png
1725620584242.png

Kati ya vitu ambavyo tutamkumbuka Mwalimu Nyerere ni ule u thinker wake. Mwalimu si tu alikuwa na maono ya kisiasa, lakini kiuongozi alikuwa kama mcheza chess. Mwalimu alikuwa na uwezo wa kufikiria mbele madhara au manufaa ya kile alichokuwa ana panga au kukipigia debe kisiasa.

Na ndio maana alipotaka kung'atuka 1980 katika uongozi, wanufaika wa uongozi wake walimsihi asubiri hadi 1985. Aliona giza lililotanda kiuongozi baada ya 1980 na miaka inyofuata. Vuguvugu la kukaribisha siasa za ushindania liziona. Lakini Mwalimu hatutamsahau kwa mipangilio yake kisiasa katika kudadavua siasa na sera.

Mwalimu aliweka msingi wa kisiasa na maendeleo na kusema kuwa, ili tuendelee twahitaji vitu vinne:
  • -Watu
  • -Ardhi
  • -Siasa safi
  • -Uongozi bora.
Watu na ardhi na utajiri wote tunavyo. Ngoma mbichi ni hapo kwenye Siasa safi na Uongozi bora.

Awamu ya pili, tatu, nne na tano kila moja zimejaribu kudadavua misingi hiyo ya Mwalimu kwa kauli mbiu nyingi za kisiasa.
  • Mzee Mwinyi - Ruksa kwa maana ya kufungua uchumi.
  • Mzee Mkapa - Ukweli na Uwazi kwa maana ya kuwa na serikali sikivu na makini
  • Mzee Kikwete - Ari mpya, Ngugvu mpya, Kasi mpya kwa maana ya kuuinua uchumi
  • Mzee Magufuli - Hapa kazi tu kwa maana liwe na liwalo kazi zitafanyika kama ilivyopangwa
Sasa tuma mama Samia na 4R. Hapa kidogo nagota maana tuna ung'eng'e ambao Tandahimba utawapa shida. Siye wasomi tutaelewa, lakini wale wa vijijini ambao ndio wengi wata husisha vipi 4R na ile misingi ya Mwalimu Nyerere.

Tunapoelekea kwenye kampeni 2025, inabidi CCM wajue wazi $R maana yake nini haswa. Matamko na kauli za Nape na yule DC mstaafu wa Longido, zimeustusha umma wa kitanzania kuwa CCM sasa hakuna common unifying Ideaology. Chama kimekosa dira hata kwa kiwango cha viongozi.

Tunajua mazingira ya Mwalimu kiuongozi siyo kama ya sasa, lakini misingi ninile ile ya kisiasa yaani maendeleo bado yanahitaji vitu vinne, watu, ardhi, siasa safi na viongozi bora.
 
Wadau mawazo yenu.
Tusisubiri matukio tu. lets think forward, kama Mwalimu.
 
Wadau mawazo yenu.
Tusisubiri matukio tu. lets think forward, kama Mwalimu.
Hapo patamu, dodoki kwanza., Kwaajili walio jiteka ama kutekwa na kama kuna marufuku ya wanao chimba dawa porini , hahahaa ila dodoki la kuchimba dawa porini lina mapicha picha, Abdul NONDO atupe uzoefu kuhusu wanaojiteka maana katajwa humu kwamba alijiteka
 
Hapo patamu, dodoki kwanza., Kwaajili walio jiteka ama kutekwa na kama kuna marufuku ya wanao chimba dawa porini , hahahaa ila dodoki la kuchimba dawa porini lina mapicha picha
Kiukweli kisiasa CCM is in a total mess.
Kila mtu anaongea lake, huyu anasema tulikuwa maporini na madiwani tumewaweka tu na mwingine anasema huko porini DC alikuwa anchimba dawa.
Nape anasema sisi ndo tunatangaza mshindi.
Kwa maneno haya CCM wanaongea upuuzi lakini hilo dilo linathibitish kuwa CCM haina unifying ideology.
 
Kiukweli kisiasa CCM is in a total mess.
Kila mtu anaongea lake, huyu anasema tulikuwa maporini na madiwani tumewaweka tu na mwingine anasema huko porini DC alikuwa anchimba dawa.
Nape anasema sisi ndo tunatangaza mshindi.
Kwa maneno haya CCM wanaongea upuuzi lakini hilo dilo linathibitish kuwa CCM haina unifying ideology.
Ndiyo maana nimeanza kwa kusema kunahitajika dodoki, to justify the so called ideology towards the coming elections. Yaani kujisafisha kabla ya kutangaza kauli mbiu changamoto waliyonayo CCM wanao pewa jukwaa kujibu kelele za wananchi hawatoshi, kwa maana wanakuwa wanaahirisha kufikiri kwa nafsi a.k.a kujizima data, maneno wanayo ongea kwa kutumia social inference unatambua kwamba kajizima data
 
Back
Top Bottom