Side effects of medication

Gorgeousmimi

JF-Expert Member
Joined
Jun 21, 2010
Posts
9,296
Reaction score
7,683
Hakuna dawa ambayo ipo pharmacetuical proven isiyokuwa na madhara(side effect).Dawa aina zote zina side effect kwa namna moja au nyingine.Kitu ambacho ni cha muhimu na tuwe makini nacho ni how IMPORTANT IS THE TREATMENT IN COMPARISON TO THE SIDE EFFECT.
Baadhi ya magonjwa ni muhimu upate tiba kuliko sideeffect,kwasababu usipotibiwa maisha yako yapo hatarini ndio maana madhara hayapewi kipaumbele.Mfano hizo dawa za uzazi wa mpango zina madhara ya kuongezeka au kupungua kwa damu ya hedhi au damu ya hedhi isiyo na mpangilio,lakutilia manani ni kwamba inakuzuia usipate ujauzito,kwahio some sideeffects we can live with them madhali hakuna madhara kiafya.
Mfano mwengine antibiotics nyingi zinachochea mvurugiko wa lactic acid bacteria kwenye tumbo/utumbo/uke hatimae kusababisha kuhara/mvurugiko wa tumbo au kuongezeka kwa unyevunyevu ukeni.Kwasababu miili yetu imejaa bacteria ambao tunaita NORMAL FLORA na antibiotics nyingi zinaua wale bacteria wenye madhara na hao normal flora ambao hawana madhara katika miili yetu(ni wazuri kiafya).Lakini tiba za antibiotics ni za muda mfupi kwahio hayo madhara yote tunaweza kuishi nayo au unaweza kula lactic acid bacterias capsules ili kurejesha/kujalizia yale mapungufu ya hao lactic acid bacterias.
Na isitoshe madhara ya dawa yanatofautiana kutoka kwa mtu na mtu.Sio wahusika wote wanapata madhara sawia ya dawa,ikumbukwe miili yetu ina react tofauti.Moja wetu anaweza apate madhara na mwengine asihisi chochote.

Side effect ni nini?

Side effect is an unwanted effect of a medication taken within normal dosage regime.
Side effect zipo za kawaida,na zilizo hatarishi kiafya.Nikisema hatarishi kiafya namaanisha yale madhara yanayoweza kuhatarisha uhai wako,kusababisha ulazwe au upate ukilema.
Side effect imegawanyika katika makundi kadhaa ambayo yamefanyiwa utafiti kutokana na reports kutoka kwa wagonjwa na studies.Nazo ni:

  1. NORMAL/USUAL:Hizi ni side effects ambazo wengi wanawaweza kupata asilimia 1% ya wagonjwa.
  2. LESS NORMAL/LESS USUAL:kati yaasilimia 0,1-1% ya wagonjwa
  3. UNORMAL/UNSUAL:chini ya asilimia 0,1% ya wagonjwa
  4. VERY UNROMAL/UNUSUAL:Wachache mno hupatwa na side effects hizi ambao ni chini ya asilimia 0,01%

Kwahio tunapo sema madhara lazima kwanza tuangalie hayo madhara yapo kwenye kundi lipi?Na je yana umuhimu kiasi gani kulinganisha na tiba ya mgonjwa.
Madhara ya dawa yanaweza kutibika vilevile.Mfano ukipata madhara ya kuumwa na kichwa,unaweza kula dawa ya kupunguza maumivu.
TUKUMBUKE DAWA NI KITU AMBACHO KINATUPUNGUZIA MAUMIVU LAKINI NI FOREIGN BODY KATIKA MIILI YETU KWAHIO LAZIMA TUWE MAKINI KATIKA MATUMIZI YAKE.
 
Asante kwa maelezo maelezo lakini sometimes hizo hizo side effects zimefanya dawa kutumika kutibu magonjwa ambayo hayakulengwa wakati dawa inafanyiwa uchunguzi. Kwa mfano viagra ilitengenezwa kwa ajili ya kutibu hypertension, wakati wa majaribio ikaonekana kuwa inaongeza stamina ya kungonoka kwa wanaume nafikiri kuanzia hapo zoezi likabadilika....
 
ni kweli kabisa uyasemayo...
 
nauliza tu ZeMarcopolo kwasababu sio kwamba kipindi chote mtu anaweza kuwa yupo Daslam tu, ndio maana nimeuliza hivyo na jamaa ikabidi akuite wewe...

Ok sawa nimekupata.

Jaribu pharmacy yoyote. Wakisema hawana waulize hylak forte - in similar effect, actually more direct effect.

Na pia ni muhimu kupata ushauri wa daktari kabla ya kutumia hizi dawa ili kuwa na uhakika wa usahihi wa matumizi yake.
 
okay, mkuu ZeMarcopolo hylak forte ni dawa inayofanana na hiyo lactic acid bacteria au ni nyingine pia?

halafu matumizi yake si jamaa amesha eleza hapo juu... kwani zina madhara pia?

zenyewe hapo juu mkuu ameshaeleza zina balance normal flora au zina madhara gani mengine?
 
Last edited by a moderator:

Haylak forte ni mchanganyiko wa hao flora. Dawa iliyoelezewa hapo juu inaweka mazingira ya flora kuzaliana lakini haylak forte ni flora wenyewe. ndio maana nimesema its actually a more direct effect.

Kuhusu madhara, well kila dawa iliyopo duniani inaweza kuwa na madhara lakini cha msingi ni kuweigh benefit ya kutumia na kutokutumia. Generally ni dawa safe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…