Sidhani kama ni sifa mwanangu kufaulu darasa la saba

MARO BM

Senior Member
Joined
Dec 31, 2011
Posts
135
Reaction score
7
Wana JF kwanza poleni na majukumu ya kila siku.
Leo nimeamua kutoa yaliyonisibu baada ya NW Mh.Mulugo kutangaza matokeo ya darasa la saba,naomba niwaulize wana JF nijisifu nini kuwa mwanangu amechaguliwa kujiunga k.1?
Nasema hivyo kwa sababu shule aliyopangiwa anapanda Magari manne(4) kwenda na kurudi ni hivyo x2,,Nauli peke yake tayari inanitoa jasho! Baada ya hayo magari manne anapanda piki piki 1500/-( pia kwenda na kurudi),Nimeshalipa malipo yao yote ila kwa sasa itanibidi nimhamishe kama hawatanipa uhamisho,vinginevyo hapa nitakuwa nafanyia kazi nauli.
Mawazo yenu ni msaada kwangu
 

Katika kata yenu hakuna ya sekondari ya kata mbona amepangiwa shule ya mbali hivyo ? Au ulihama eneo la kuishi. Anyway, suluhisho ni kumhamishia katika shule ya karibu ili kuepuka usumbufu wa usafiri kwa mwanao na gharama kwako kama mzazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…