Sielewi nimepatwa na nini mwenzenu...

....Haya mazee kwa kuwa uliomba senksi nimekugongea kivile tu ni wa humu humu. Otherwise umeongea mengi nikipima naona mzani unakuja kwangu...Sorry kama nimekukwaza!!!
 
...Acha hasira bht...msimamo upo tena wenye akili nadhani kama ni majaribu nimeshakumbana nayo wa kwetu...mtoto nilizaa na mdada mwingine. Tulishindwana tu.
 

mwanaume wa principles/morals...mie ndio nishakupenda tayari!!!!!afu siku hizi napenda penda tu....ukiwa na nyodo kama Nyani Ngabu mie nakuzimia!...ukiwa mcheshi kama X-pin mie unaniacha hoi...ukiwa na hekima kama De Novo mie ndio kabisaaaaaaaaaaaaa...nadhani nina pepo na wanaume wa JF!...mnalo!!!!!!!!!!!!!!!!?!
 


Siyo tu jukwaa la mapenzi limeingiliwa bali Jamii imeingiliwa hakuna mijadala inayoendelea hapa kutwa kucha ni mapenzi tu kama ilivyokuwa huko nyuma. Watanzania tuna matatizo makubwa sana kama kila tunapoamka na kulala hatuwazi kingine chochote ila mapenzi tu. :angry:
 
pole
lakini kumbuka kuwa Mungu aliumba na anaendelea kuumba vizuri tu,
vibaya ni vya shetani, hivyo angalia sana kwa tabia yako unayoenda kuianzisha
ya mapenzi ya hovyo na kutokuwa na msimamo,
tamaa ya itaiangamiza na roho pia, hapo huna lolote ila wataka kuifurahisha nafsi yako tu,
kumbuka kuifurahisha nafsi, kunaiua roho na mwili pia kisha kuipoteza kabisa
 
huna msimamo wewe, ogopa sana Arusha watu wa kule wako kibiashara zaidi na ni wazuri ili awachelewi kukuchenjia, inaonekana wewe ni mgeni wa mapenzi ndio maana umechanganywa na mtu wa kupita aliyekukubali kirahisi (loose ball) na kukutega ili uingie line, fumbuka MBAYUWAYU wewe utapata laana bure kutoka kwa wazazi kwa tamaa za muda mfupi

Mapenzi ni vitu vingi sana sio sura wala pesa kama unavyofikiria na hilo JOTO (HOTNESS) ni akili yako mwenyewe inacheza wala si huyo m/mke, zinduka, amka, kimbia achana na huyo shetani na majaribu anayokuletea ama vp badili namba za simu kabisa umpotezee

wanawake ni wengi sana lakini mke mwema ni mmoja tu ambaye ni huyo mchumba wako wa awali

Halafu hapa umekuja kuomba ushauri umwache huyo mdada wa Arusha au umekuja kumsifia? tupe jibu. Hii sehemu tunawekana sawa lakini atutoe ushauri wa kukupoteza wewe ZINDUKAAAAAAAAAAAA
 
Halafu jamaa anashauriwa anakuja juu sasa umeleta topic hapa ya nn? watu wanaumiza vichwa kukusaidia unaleta ujuaji

WEWE NI SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA umeshapotea
 
1.umekutana na mjanja,jasho litakutoka.
2.yaani huyo bibie ninavyoona unaweza kumsindikiza hata guest akamegwa wewe unasubiri nje pasipokujijua.
3.Nahisi uwepo wa pepo hapo.........maombi yana hitajika.
4.Samahani,lakini mzee kwa staili hii una safari ndefu sana ya kutafuta MWENZA.
5.Uliekaa nae angalau kwa mwaka na nusu kama mchumba huyo NDIE.
6.wasichana wazuri na warembo hawaishi kwa taarifa yako na wengine hata kuzaliwa bado.
7.Sasa? je ungeenda maeneo ya mbulu,babati,mto wa Mbu je?ha ha ha ha ha,USINGERUDI dar.
8.Eti nini?umkaribishe DAR,naona una hamu ya kuishi na pepo,utachunwa ngozi.
9.Akili yangu inaniambia kuna kitu umelishwa wakati fulani mkiwa wote pale Arusha,kumbuka vizuri,eeeeeh unakumbuka eeh,YES.nguvu za GIZA
10.Usipende sana DEZO hasa toka kwa akina mama,kwanini akusomeshee mwanao? we hushangai?
hata hivyo ndugu yangu,hayo ni mawazo yangu binafsi, TUSAMEHEANE KAMA NAKUKWAZA si unajua tena? dawa(ushauri) zingine chungu
kuzimeza lakini ni single DOZE unapona.Hapa nimekuandikia drip ya kwinini naona homa yako kali sana,MARALIA 8.MWELEZE MCHUMBA WAKO UNAETAKA KUMWACHA AKUKOLOGEE UJI UNYWE DAWA IFANYE KAZI VIZURI. UMENIELEWA?
 
Hivi wewe, umeshakuwa na wapenzi wangapi mpaka sasa? Umetuambia tu mautamu wa huyo wa Arusha, lakini what's wrong with the one u were about to marry? Anyway, nakushauri umwache huyo mpenzi wako wa siku nyingi na umuingeji huyo mpya wa Arusha uliyekuwa naye kwa siku mbili tatu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…