Siioni amshamsha ya Forex, vipi watu wameshapigwa?


kwakifupi "watanzania wanapenda maendeleo lakini wanawachukia watu wenye maendeleo"
 
Nilisoma habari ya forex ikanivutia sana nikawaza lazima nitakuja kuifanya hii biashara siku moja.

Katka mishemishe zangu nilibahatika kwenda south afrika
Katika eneo nililokuwa nafanya kazi kulikuwa na dada mmoja m xhosa ambaye anaonekana kasoma mjanja mjanja hivi tulikuwa tunapiga stori nyinginyingi tu kaniambia siku moja anafikiria kuja tanzania zanzibar nikamkaribisha nikamuelezea na mambo mengine asiyoyajua kuhusu iyo tz na zanzibar
Kwa sababu mara nyingi tulikuwa pamoja,siku moja nilimuuliza kama anaifaham Fx aliniambia anaifaham sana na amewahi kufanya hiyo, nikamwambia katika ndoto zangu ni kuja kufanya hiyo biashara nikaomba msaada kwake anifundishe. aliishia kunishauri niachane kabisa na mawazo hayo kaniambia ile ni kama kamari yeye kaishia kupoteza pesa nyingi na mali zake hataki hata kuisikia.kaniambia ili kuwa broker inabidi kuwa muongo wa muda wote hapo ndipo wazo la fx liliponiondoka ila bado nitatafuta ukweli zaidi kuihusu hii
 
frex is not for every one...bora huyo mxhosa wako aendelee na biashara yake ya kuuza unga
 
Isije ikawa ndo ile mtu unapigwa, unatulia kimya
 
Hahahaaa mbona watu mnaiongelea sana hii ishu? Kama mnaona utapeli waacheni wenyewe wamesha kubali kutapeliwa, nyie fanyeni yenu. Au ndio Yale ya sizitaki mbichi hizi?!
Mbn unapanic bro
 
Naamini moja ya njia nzuri ya kufanikiwa ni kujifunza kwa waliofanikiwa.Huwezi kufanikiwa kwa kufurahia matatizo ya aliyefanikiwa.
 
Mkuu mwenyewe nimekuwa bize zaidi ya advance. Hata mpaka wife analalamika simkamui vizuri mana energy Zote zimeenda kwa forex

Mkuu nilidhani ni mimi tu peke yangu nimeliona hili. Ni kweli kabisa once you make a decision to enter into this biashara ratiba nyingine zinakupita kabisa.

Niko katika hatua ya kumaliza kusoma vitabu na imefika hatua nimekuwa nikisahau hata menyu ya TigoPesa na Mpesa *150*01#/*150*00#....
 
Sasa kama hela ya huko ni ngumu sana.. Kwann wasifanye haya rahisi kwanza.. Trade! (For instance) manufacturing?! Afterall I see more billionaires from simple things and none from forex!

Kwanini mtu aache kufanya kazi ngumu inayomuingizia 80,000 kwa siku ili afanye kazi rahisi inayomuingizia 10,000 kwa siku?
 
Kwanini mtu aache kufanya kazi ngumu inayomuingizia 80,000 kwa siku ili afanye kazi rahisi inayomuingizia 10,000 kwa siku?
Unasema kweli mkuu. Mwisho wa siku nadhani kinachokuwa muhimu ni volume.. Na that has been name of the game for centuries..

Ingekuwa ni kuangalia value migodi ya dhahabu na almasi tu ndio ingekuwa matajiri.. Fun enough naona hata watengenezaji wa pin wanaendelea kuwekeza despite faida yao kuwa ndg sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…