Elections 2015 Siioni sura ya Magufuli,migiro wala amina kukemea ufisadi ulioko kwenye system!

Elections 2015 Siioni sura ya Magufuli,migiro wala amina kukemea ufisadi ulioko kwenye system!

MWANAKB

Member
Joined
Jun 21, 2015
Posts
51
Reaction score
18
Narudia tena kuwa sioni kama kweli sura hizo zina ubavu wa ku-reform system iliyokwishajengeka ndani ya serikali hii ya Tanzania. sioni kama mmoja wao kati ya hao anayesubiriwa kuteuliwa kukiuza CCM kuwa anaouwezo wa kukemea uzembe wa baadhi ya watumishi wa umma, mwenye uwezo wa kukemea ufisadi uliokithiri ndani ya Tanzania hii! CCM wamejiloga wenyewe! kwangu mimi Magufuri ni WAZIRI MKUU au anafaa kuongoza wizara na si nchi. MIGIRO sioni hata kama anatosha ndani ya wizara achilia mbali nchi. Magufuri ni mtu wa maamuzi ya haraka haraka bila kutafakari kitakachotokea mbele baada ya maamuzi. Hata hivyo, sioni kama anao uwezo wa kuwakemea viongozi aliofanya nao kazi ndani ya serikali kwa muda mrefu sana. Naona sura ya kuwafumbia macho pindi watakapovurunda au hata kushiriki ufisadi. Niona sura ya kuwavumilia kina Simbachawene wanaojimilikisha mafuta na gesi kwa kupitisha miswada kwa dharura. SIIONI SURA YA KUKEMEA UFISADI KATI YA HIZO TATU BORA WALIZOLETA. Kwangu mimi labda angekuwa mzee wa busara MWANDOSYA! Kidogo huyo sura ya UONGOZI WA JUU KABISA ANAYO, kama ilivyo kwa Dr. Slaa, Walioba, A. Ramadhani. Hivyo kura yangu imebaki kwa Dr. Slaa endapo atapitishwa na upande wa pili.
 
Tumeshakujua Wewe Ni TEAM NIMEKATWA Na NINA HASIRA ( EL ). Pole Sana!
 
Tumeshakujua Wewe Ni TEAM NIMEKATWA Na NINA HASIRA ( EL ). Pole Sana!

hapo umekosea sana mkuu, ki ukweli namkubali sana Mwandosya naona ana maamuzi yaliyotulia na hayumbishwi hata hivyo tumuombee kila la kheri Msomi na mwanasayansi Dr. J.P.MAGUFURI katika safari yake. Ngoja tungoje UKAWA nao wanatuletea nani
 
hapo umekosea sana mkuu, ki ukweli namkubali sana Mwandosya naona ana maamuzi yaliyotulia na hayumbishwi hata hivyo tumuombee kila la kheri Msomi na mwanasayansi Dr. J.P.MAGUFURI katika safari yake. Ngoja tungoje UKAWA nao wanatuletea nani

Wanatuletea Mgonjwa Mwingine Na Bingwa Wa Kuvunja Ndoa Na Kuoa Hovyo Hovyo Na Naambiwa Hivi Majuzi Alienda Kutibiwa Tena Ng'ambo.
 
Wanatuletea Mgonjwa Mwingine Na Bingwa Wa Kuvunja Ndoa Na Kuoa Hovyo Hovyo Na Naambiwa Hivi Majuzi Alienda Kutibiwa Tena Ng'ambo.

hayo mambo ya ndoa sasa aaahh. hayo ni ya kibinafsi zaidi mkuu. nahis hata wewe hapo ulipo hujawa na mmoja tu.
 
Back
Top Bottom