Sijaelewa nini kimetokea!

shibela

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2018
Posts
1,068
Reaction score
3,507
Alfajiri ya Leo kwenye saa 11:30 hivi natoka nyumbani naenda kwenye mihangaiko yangu! Nilikuwa upande wa magari yanayorudi toka mjini! Upande wa magari yanayoenda mjini kulikuwa na msururu wa magari, gari ya mwisho ilivyomalizikia ghafla mbele yangu upande huo nikaona jeneza katikati ya Barabara nikafikicha macho labda sioni vizuri jamani ni jeneza kabisaa jeneza!!!na nilikuwa kwenye 40km/h yaani nimeona vizuri kabisa,Sasa sijaelewa lilikuwa linasafirishwa limedondoshwa kama limedondoshwa ina maana waliokuwa nalo hawajaona??? Sielewi nini kimetokea au kama kuna mtu alishawahi kukutana na situation kama hiyo wananzengo!!
 

Siti ya mbele kabisa...ngoja waje
 
Hatari... Barabara ipi hiyo?
 
Mkoa gani huo ulipo ili nianze utabiri wangu uchwara?
 
Mkuu ninachojiuliza kama lingekuwa upande wangu ningefanyaje,ningepita nalo?ningesimama?ningelikwepa?
Inabidi upite nalo..alokufundisha kudrive hakukwambia mambo yanayofanana na hiki ulichokutana nacho na namna ya kukabiliana nayo?
 
Mkuu ninachojiuliza kama lingekuwa upande wangu ningefanyaje,ningepita nalo?ningesimama?ningelikwepa?
Kitu Chochote unachokiona barabarani ambacho sio kawaida Sheria ni moja tu kupasuka hata kama unamuona mama Yako porini barabarani usikuu wewe pasua ukitaka kukwepa ndio itakuwa mwisho wa maisha Yako..na ukifa unaenda kuzimu sio mbunguni
 
Mjini ya Mkoa,wilaya,au kijiji kipi?? Maana hata huju kwetu Kantalalamba na Kigurunyembe ni mjini.
 
Inabidi upite nalo..alokufundisha kudrive hakukwambia mambo yanayofanana na hiki ulichokutana nacho na namna ya kukabiliana nayo?
Darasani vs field my dear hapo kwenye kupita nalo hapo!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…