Zanzibar 2020 Sijasikia the so called "ubeberu" Zanzibar kwenye kinyang'anyiro cha Urais

Zanzibar 2020 Sijasikia the so called "ubeberu" Zanzibar kwenye kinyang'anyiro cha Urais

Ramea

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2015
Posts
2,146
Reaction score
4,084
Beberu ni Mbuzi dume, hii ni tafsiri sawia kwa Mtanzania wa kawaida wa kule Nyololo na Nanjilinji. Sifa kubwa ya beberu huyu, ni kupiga kelele usiku kucha, kunusa mikojo ya majike zizini na kuwa na harufu kali ya mwili.

Kuna beberu yule wa kikoloni, wakoloni katika hatua ya juu ya ubepari wao, waliitwa mabeberu. Hawa ndiyo ambao walikuwa maadui wa nchi za kiafrika hadi kipindi Cha uhuru miaka ya 1960's.

Ingawa uadui huo uligeuka kuwa urafiki baada ya uhuru na hasa baada ya kuanguka kwa Soviet Union. Nchi nyingi ziliendelea kuwa na urafiki na watawala wao chini ya miavuli Kama ya Francophone states zilizokuwa chini ya wafaransa na nchi nyingine chini ya jumuia ya madola, kwa makoloni ya kiingereza.

Turudi kwenye mada, adui na agenda kuu ya Tanzania yetu sasa hivi ni "ubeberu" tulianza na uchochezi na uzalendo Kama defensive mechanism. Vikashindwa ingawa wachochezi na wakosa uzalendo wameteseka na pengine kufungwa na kupotea kusikojulikana.

Najaribu kujiuliza, kwanini utitiri wa kuchukua fomu ya Urais Zanzibar usiangaliwe kama Kuna mkono wa Mabeberu Kama ilivyo agenda kuu Tanzania Bara? Kwanini tusiwaite wachochezi watia nia wa Urais wa Zanzibar? Kwanini tusiwaone kuwa wakosa uzalendo? Najaribu kuwaza kwa sauti.

Nadhani Mabeberu wa Tanzania Bara ni wazungu, wakati mabeberu wa Zanzibar ni Mbuzi dume, Yule anayenusa mikojo ya majike na kunuka mwili.
 
Sera ya kupambana/ kuogopa mabeberu au wanaoitwa mawakala wa mabeberu ni ya CCM. Tuwaulize, tangu lini tukawa mbuzi jike,hadi tuogope mabeberu na kujaribu kufunika vikojoleo kwa vipande vya mikia?

Hii ni nchi Huru yenye kila haki ya kujiendeleza kiuchumi, kijamii,kisiasa nk bila kuogopa beberu au kingine chochote.Watawala wasitafute visingizio vya mabeberu/wapinzani kila wakishindwa kutekeleza wajibu wao.

Uungwana ni kukiri udhaifu wa kiutendaji kama ukitokea na kukubali mawazo/ hoja mbadala na siyo kutafuta visingizio.
 
Sera ya kupambana/kuogopa mabeberu au wanaoitwa mawakala wa mabeberu ni ya CCM.Tuwaulize,tangu lini tukawa mbuzi jke na kujaribu kufuniko vikojoleo kwa kipande cha mkia?
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hayo yanafanyika kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar au ya JMT?Kwa kufanya hivyo ndiyo usahihi wa jambo hilo la Rais wa Zanzibar kuchaguliwa Dodoma na CC na/au NEC ya CCM?

Miongoni mwa hao wajumbe wa hivyo vyombo vya maamuzi ni Watanganyika(TZ Bara),ni sahihi kuwaamulia Wazanzibar nani awe Rais wao?Hii inatofauti gani na ukoloni/ubeberu mnaoupiga vita?

Yumkini uwezo wangu wa kuelewa una upungufu,lakini misingi ya JMT imevurugwa kiasi kuwa sasa hivi ni vigumu kuelewa nchi hii inaelekea wapi?
 
Beberu ni Mbuzi dume, hii ni tafsiri sawia kwa mtanzania wa kawaida wa kule Nyololo na Nanjilinji. Sifa kubwa ya beberu huyu, ni kupiga kelele usiku kucha, kunusa mikojo ya majike zizini na kuwa na harufu kali ya mwili.

Kuna beberu yule wa kikoloni, wakoloni katika hatua ya juu ya ubepari wao, waliitwa mabeberu. Hawa ndiyo ambao walikuwa maadui wa nchi za kiafrika hadi kipindi Cha uhuru miaka ya 1960's...
Kule Zanzibar kuna WAHAFIDHINA. Hujawasikia hadi leo? Fungua Zanzibardaily.com
 
Duh...!.
Beberu ni mbuzi dume, ubeberu sio kule kunusa, tena unadhani ni ananusa pee!, no!, ni anapima joto, heat, akikuta mbuzi jike yuko kwenye heat, anachofanya beberu ni kumpanda, no negotiations!, kama afanyavyo Jogoo la kuku, hata kama mbuzi jike au kuku mtetea hataki, atakimbizwa hadi achoke na atoe kwa lazima. Ile hali ya kujitwalia bila ridhaa ndio ubeberu.

Kwenye human development index tunaanzia kwenye ujima, communism, ukaja ukabaila, na ubwanyenye, ukaja ubapari, capitalism, the highest stages of capitalism ni imperialism, huu ndio ubeberu, ulifanywa na wakoloni during colonial era, na baada ya nchi nyingi kupata uhuru, imperialism iliendelezwa kupitia neo colonialism, ukoloni mambo leo....
Mkuu leo ndo kwanza useme. Hii ndo Tanzania ya leo na Wazanzibari wanaojiita wenyewe wamekaa kimya wakichekelea wakidhani wanamkomoa mtu, ila kuna siku wataamka kutoka usingizi mnono - wenyewe wanauita usingizi wa pono.
Z
 
Beberu wa Zanzibar ni Tanganyika ambae anawaamulia wazanzibari nani awe rais, na kumfanya rais wa Zanzibar kama poppy
 
Nalikumbuka lile bango la "Machotara Hizbu, Zanzibar ni nchi ya waafrika"

Huko kuna Machotara HHizb!
 
Back
Top Bottom