Sijawah kufanya biashara na nina mil 1.2 nifanye biashara gani ..??

covid 19

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2014
Posts
6,967
Reaction score
17,452
Wakuu nimejichngisha na nimepata 1.2 nifanye biashara gani coz sijawah hata cku moja kufanya biashara naomb mawazo yenu wakuu nipo hapa Dsm...!!
 
Fungua genge la ndizi na mbogamboga linakufaa,kwa mtu mweledi wa mambo hubuni jambo na kutafuta ushauri na si kuomba msaada wa kubuniwa jambo,duh hata hilo genge litakushinda wewe!
 
Fungua genge la ndizi na mbogamboga linakufaa,kwa mtu mweledi wa mambo hubuni jambo na kutafuta ushauri na si kuomba msaada wa kubuniwa jambo,duh hata hilo genge litakushinda wewe!

maskini majibu yako yanavunja moyo, umemshaur then umemponda!
 
usijali unaweza kupata ushauri.unajua biashara mara nyingne inategemea na mazingia ulipo! sbb hapa unaweza ambiwa ufungue bar zanzbar!!! so anza mwenyewe kutafakar hapo ulipo unaweza kufanya nini?!
 
Fungua genge la ndizi na mbogamboga linakufaa,kwa mtu mweledi wa mambo hubuni jambo na kutafuta ushauri na si kuomba msaada wa kubuniwa jambo,duh hata hilo genge litakushinda wewe!

Ukikaa bila kutuma post unawashwa nini km huna cha kusema si upite tu....oovyoooo kabixa..!!
 
usijali unaweza kupata ushauri.unajua biashara mara nyingne inategemea na mazingia ulipo! sbb hapa unaweza ambiwa ufungue bar zanzbar!!! so anza mwenyewe kutafakar hapo ulipo unaweza kufanya nini?!

Ok poa...!
 
kiuhalisia kusema ufanye aina gani ya biashara ni ngumu ila naweza kukupa mawazo halafu uangalie mwenyewe,pata

wazo la biashara kwa kuangalia eneo ulilopo mfano labda nyumbani unapoishi angalia ni kitu gani kinakosekana

hapo mtaani kwenu na hicho kitu kinahitajiwa sana na wengi na wakati mwingine hulazimika kukifata mbali,ukipata

hicho kitu hiyo ndo biashara yako na hakika utapiga hela sana mpaka wengine waje wakuige wewe utakuwa mbali

sana. Pia unaweza angalia mazingira mengine mfano mahali unapotumia muda mwingi kukaa angalia hilo eneo lina

uhitaji gani,eneo lolote tu lichunguze lina uhitaji gani ukitumia hiyo fursa vizuri umetoka.Usijali hata kama

hiyo biashara unaona si hadhi yako wewe fanya usione aibu hapo ndo mafanikio yako.


Pia unaweza angalia ujuzi gani ulionao,huo ujuzi ugeuze uwe biashara wekeza hapo utaona matunda yake.
 
Wakuu nimejichngisha na nimepata 1.2 nifanye biashara gani coz sijawah hata cku moja kufanya biashara naomb mawazo yenu wakuu nipo hapa Dsm...!!

Hakuna jambo gumu kama kumshauri mtu usiyemjua afanye aina gani ya biashara hata kama Ana Mtaji kiasi gani...
Elimu yako? Umri? Ujuzi? Nk ni muhimu
 
Nunua line ya m-pesa kwa laki 6, laki 6 nyengine ifanye iwe mtaji (ni ndogo sana ila hamna jinsi) kama utaweza kujinyima yale yasiyoyalazima utaona mafanikio
 
Ebu kaa hapo bar agiza Kilimanjaro na kiti moto acha kuwaza ujinga
 
asante mkuu nayashughulikia mawazo yko na nita kujurisha unishauri zaidi.
 
kuna jamaa anajiita Kigogo
anjifanya anahela sana
 
Last edited by a moderator:
Nunua chupa kubwa za chai, uza uji wa ulezi sehemu zenye mikusanyiko yawatu wengi kama vituo vya daladala n.k. Uza asubuhi na jioni soon utakuwa kama Bakhresa.
 
Nunua chupa kubwa za chai, uza uji wa ulezi sehemu zenye mikusanyiko yawatu wengi kama vituo vya daladala n.k. Uza asubuhi na jioni soon utakuwa kama Bakhresa.

na chapati mkuu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…