Sijawahi kutambua harufu maishani mwangu, je kuna Tiba ya kuweza kutambua harufu?

Doctizo Mtengwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2019
Posts
828
Reaction score
1,513
salam kwenu wana jf.
wakuu kama kuna anayejua hiyo tiba naomba anisaidie ,au aliyewahi kupona tatizo kama hili la kutokusikia harufu naomba mwongozo wa tiba hili tatizo nimezaliwa nalo ,kwani sijawahi kusikia harufu maishani mwangu .Harufu kwangu ni kitu nilichoambiwa kipo kwa anayejua tiba msaada tafadhali...
 
Duh nenda hospital inamaana olfactory nerves hazina tena ushirikiano na ubongo


Mkuu itabidi niende tu ,mana nahitaji kusikia harufu toka mda mrefu ila sijawai fanikiwa kuskia, na "olfactory nerves" kama ulivyo sema hazina ushirikiano na ubongo ,je kuna madhara mkuu naeza pata kwa kutokuskia harufu.
πŸ‘‰πŸ‘πŸ‘
 
Pole sana...
Kwa maana hiyo hata ladha ya vitu husikii pia...
Cc: mahondaw

asante mkuu,
yani ukinipa kitu ambacho sijawai tia kinywani siwezi kukitambua kwa ladha ... ata mda mwingine ladha kwangu sio kitu cha kuzingatia sababu kuzitambua inanichukua mda
mf. Mboga za majani zikipikwa siwezi tena kujua jamii yake ...
Mkuu utanisaidiaje tu maana nimeshaichoka hii hali
 
Ndio n muhmu sema ukimuona daktar atakusaidia na ikishindikana bas atakupa maelezo ni kama ambavyo mtu hasikii au kuona ila anaishi tu
 
Ndio n muhmu sema ukimuona daktar atakusaidia na ikishindikana bas atakupa maelezo ni kama ambavyo mtu hasikii au kuona ila anaishi tu

nitatafuta suluhisho mkuu kukubali haiwezekani kirahisi ...
 
Kama unaishi Dar acha tu mkuu,kuna maeneo yananuka sana pia kuna watu wanajipulizia marashi makali sana wala usitafute kuyajua tunayoteseka nayo sisi.
 
Kama unaishi Dar acha tu mkuu,kuna maeneo yananuka sana pia kuna watu wanajipulizia marashi makali sana wala usitafute kuyajua tunayoteseka nayo sisi.

πŸ˜€πŸ˜πŸ˜
ila kuna vitu nitavikosa mkuu , naskia kuna vitu vina harufu nzuri sana kingine ni kuwa wife akiunguza apo jikoni sitaki iwe siri yake tuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…