Habari wana jf wenzangu mm n kijana mwenye umri wa miaka 18 nasumbuliwa na tatizo la kutoa uchafu mweupe wenye utelezi ambao hauna harufu kwenye uume baada ya kukojoa ila wakati nakujoa kunakua hakuna maumivu yoyote na uchafu huu hutoka endapo tu nikiwa natoa haja kuja pia mkojo wangu umekua wenye harufu mbaya sana. Mwanzon hali hii ilipojitokeza nilienda hospitalini doctor akanipa dawa za gono hali hii ilibaki palepale na tena vipele vikajitokeza kwenye korodan baada ya kurudi tena hospitalini daktari akanipa dawa za fungus. Baada ya kutumia dawa hizi hali ya vipele ndo ikazidi ndipo daktari akanipima mkojo ndipo akasema nina UTI (urinary track infection) akanipa dawa pamoja na sindano baada ya wiki mbili vipele vikakauka lakin uchafu huu bado upo na siku hadi siku uchafu unazidi kuwa mzito na viungo vyangu vya mwili vimekua vikilegea na kua na maumivu kwa mbali. Nisaidien jamani nn nifanye maana huu ni mwaka wa tatu nikiwa nahangaika