Sijui kwanini nimeumia hivi

Sijui kwanini nimeumia hivi

Habari za asubuhi wanajf

Iko hivi... Nina rafiki yangu ana mtoto( naweza nikasema ni single mom) ila isieleweke vibaya, nilisomaga nae olevel huko ila nikama bahati tu tumejikuta tunaishi tena mtaa mmoja.

Ijumaa jioni wakati natoka tu ofisini alinipigia Simu akaniambia anashida kama naweza nipitie nyumbani kwao nikamuone, kwakua nilikua sina ratiba nyingine nikasema isiwe tabu kabla sijafika nyumbani nikapitia...
Nilimkuta yuko good ila mwanae alikua anaumwa sana ile mtoto kazidiwa na akaniambia ameshindwa kwenda hospitali hana ela na almost kila aliyempigia simu wamemuahid tu tangu asubuhi na hakuna aliuemtumia mpaka mda huo sa1 jioni inaelekea saa2..

Kiukweli sikua na hela and i was totally broke,, yaani wiki ile iliyoisha mwenyewe nimeishi tu kwasababu nina wazazi maana nilikua nina mambo mengi yananihitaji hela kiasi kwamba sikua nimebakiwa na hata Mia mbovu.... Lakini nikasema kwenye suala la kuokoa maisha ya mtoto isiwe kesi nikamwambia ngoja nirudi kwanza nyumbani, nikamsimulia mama tukaongea na dada yangu wakasema tu hapa kwa harakaharaka hatuna namna tumdanganye tu mzee kitu chochote jioni hii atupe hela.. kweli mzee bila hiyana tukamshawishi akanipa 150k nikamfata kwao tukaenda hospitali usiku uleule...

Mtoto akapewa huduma ya kwanza na baadhi ya vipimo wakamlaza ili asubuhi aendelee na matibabu mengine( mda wote huo anawapigia ndugu zake wakiwemo na baba wa mtoto hata simu hawampokelei wengine), asubuhi yake niliomba tu ruhusa kazini nikawaambia nitachelewa ili nione mtoto atakua anaendeleaje....
Case ya mtoto ikawa kubwa wakasema tuende nae hospitali nyingine kubwa ( Peramiho nadhani watu wa songea wanaijua), kuna vipimo alivyoambiwa wampime vilikua vinahitaji hela almost kama laki2 tena nikamwambia mama akanitumia tukafanikisha.. Kwasababu kazini nilikua wanapigapiga sana simu na nikaona wanaendelea vizuri na mama yake alikua ashafika nikamwambia naenda ofisini incase kimetokea chochote utatuambia nikampa na namba ya mama kama mimi nisipopokea ampigie,, nikaondoka. The bad thing is nilikua busy busy sana hadi siku ikaisha sikuwatafuta tena..

Kinachoniumiza ni kwamba, jana mchana nilimpigia simu hakupokea nikaenda kwao sikukuta mtu, nikaenda hadi peramiho tena kulivyo mbali nikaambiwa wameruhusiwa na hakunipa taarifa.... Kuanzia jioni nimeingia WhatsApp naona ameweka status nyingi nyingi kufungua nikawa naona amescreenshot miamala yote ya watu waliokua wanamtuma hela na kuwapa credits Mungu awabariki sana kwa kuokoa maisha ya mwanae maana alikua kwenye hali mbaya sana na nini nini.. Screenshot kama kumi hivi na kitu na amewataja na majina kabisa...

Cha ajabu hiyo miamala hakuna hata wa mtu mmoja uliofikia hata 30k, wote ni hizo hizo tu efu10 ef5 ef7, kawaandikia macaption mazito mazito.. Nimebaki najiuliza mbona alikua ananiambia hawapokei simu, na hela inaonekana walimtumia sikuileile ambayo aliniambja na mimi niende kwake kumuona,,.. Mimi ambayo nilikua nae kuanzia siku ile hadi usiku nikaacha na kwenda kazini na tumeclear bills zote hata asante hajaniambia na wala taarifa kama wameruhusiwa hajanipa. Nimesubiri jana yote hadi leo saizi hajanipigia hata simu, Kina mama wananiuliza wanaendeaje nawaambia tu wanaendelea vizuri huku roho inauma..

Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee😥😥
Tenda wema nenda zako. Moyo wa mwanadamu ni ngumu kuuelewa.

Ndio maana tunasisitizwa kuwatreat watu kulingana na mioyo yetu ilivyo, na sio kulingana na wanavyotutreat au mioyo yao ilivyo.
 
Nimetenda wema nimeenda zangu wakuu, lakini bado roho inaniuma aisee😥😥

Siku zote mtu "masikini" usimsaidie masikini, acha masikini asaidiwe na tajiri...

Huku mtaani wanakwambia, gari bovu haliwezi kulivuta gari jingine bovu...

Hili ndilo la kujifunza.

NB: Usiielewe vibaya hiyo masikini niliyoiwekea " "...
 
Siku zote ishi kwa kusaidia bila kutegemea malipo yeyote. Iwe ya shukrani ama chochote.

Kwa sababu hata shukrani isingekuongezea chochote.
Yaani nashindwa kueleza ninavyojiskia,, sihitaji anilipe chochote wala chochote ila tu nimeumia ndomana najishangaa kwanini inakua hivi hadi nashindwa kujizuia.. Hata sielewi naumia nini yani
 
Nimeumia sana mkuu, ameshindwa kunishukuru basi hata angenipigia Simu anijulishe kama wanaendelea vizuri.. Nimeumia haki ya Mungu tena[emoji3064]
Mkuu samehe bure hili sadaka iwe sadaka inatakiwa uiotoe mazingira yanayo uma rafiki yako kazingua Mungu pia anaona lakini wewe utapata sawabu kupitia yeye samehe shida pia hazijawai kuisha
 
Binadamu muda mwingine ni shida tu mshukuru Mungu umekuwa sehemu ya kuokoa maisha ya mtoto wake shida haziishi. Mie niliwahi kumtafutia kazi rafiki yangu kwenye kampuni nayofanyia kazi na alikuwa kwenye wakati mgumu yeye na familia yake lakini baada kupata kazi akaanza kunipiga majungu kwa maboss nikaishia kupoteza
 
Binadamu muda mwingine ni shida tu mshukuru Mungu umekuwa sehemu ya kukojoa maisha ya mtoto wake shida haziishi. Mie niliwahi kumtafutia kazi rafikinyangu kwenye kampuni nayofanyia kazi na alikuwa kwenye wakati mgumu yeye na familia yake lakini baada kupata akaanza kunipiga majungu kwa maboss nikaishia kupoteza
Pole sana aisee
 
Back
Top Bottom