Akili Kichwani
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,508
- 220
- Thread starter
-
- #21
Namtakia kila la heri...Kila jambo lina wakati wake na MUNGU hufanya kwa makusudi kabisa ili yeye atukuzwe Milele..Wala hahitaji faraja kwa sasa kwani huzuni na mateso vilishaisha...Ana bahati kwani amepata hata fursa ya kusoma PHD wapo ambao wanatamani lakini hawataweza kufikia malengo hayo kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao.
I have been here before.. de javu!
Mungu amuinue
Amsimamishe juu ya miamba
Amkinge na maadui wajao kama rafiki
Amponye na mkono wa mtesaji
Ampe furaha alalapo na aamkapo
Amwagie baraka zake kwa mujibu wa Kumb. 29
Na amletee karibu yake marafiki wa kike na wakiume
Ambao ni ndugu kuliko wale wa damu
Ambao hawatamuacha upweke; katika giza na katika nuru
Katika mvua na kati hari
Katika majanga na katika ya neema
Katika huzuni na katika furaha
Katika yote yaliyo mema.
Siku hii ambayo nilikuwepo leo.. ninamuinua kwake yeye Baba wa Mianga ambaye kwa jina lake "ubaba wote mbinguni na duniani" unaitwa!