Sikiri Mimi Maskini

[QUOTguasa;8834572]duh!enzi za chilunda apambana na chui,lindu amuokoa kapilima ah kitambo.[/QUOTE]

Naaam!ulikuwa ni usiku wa giza nene na mawingu ya mvua,wakati chilunda alipopambana na chui,chilunda si kijana Mwoga,alikata shauri kwenda ngomani ingawa kulikuwa na giza.
 

Mkuu Bujibuji fanya editing kidogo,aliyekuwa analialia ni Sikili,mdogo wake aliyekuwa anakula bata home ni Sadiki.
 
Last edited by a moderator:
Huyu ni baba
Baba ana ng'ombe,
ngo'mbe wake ni mwesi,
Baba anasema,
Kimbia ng'ombe,
kimbia upesi,
Kimbia nyumbani
Baba ana njaa.
 
Hii ni special kwa wazee wenzangu tu.
kama wewe hukuwepo wakati huo soma upate idea tulikuwa tunafaidi nini!
Tulipokuwa primary,unakumbuka?
Tujikumbushe kwa Upande wa vitabu vya Kiswahili, as huko nako ilikuwa burudani tupu. stori kama KIBANGA AMPIGA MKOLONI, SIZITAKI MBICHI HIZI,SIKU YA GURIO KATERERO,BENDERA YA TANZANIA,ANDUNJE( mtoto mdadisi), NGANENEPA ANG’ATWA NA NYOKA,AHADI KUMI ZA MWANA TANU na nyingine nyingi zote ilikuwa burudani tupu.
Kweli wakati ule mtaala ulikuwa umetulia, kwa sasa hivi sifahamu mitaala ikoje lakini nakiri mtaala katika somo la kiswahili, ulikuwa umetulia.
Nimalizie kwa beti ninazozikumbuka( japo sizikumbuki vizuri sana) kutoka katika shairi la sizitaki mbichi hizi
Hadithi inayokuja, ni ya sungura sikia
hadithi uliyongoja leo ninakuletea
Alitoka siku moja njaa aliposikia
njaa aliposikia sungura nakuambia
Siku hiyo akaenda porini kutembelea
akayaona matunda mtini yameenea
sungura akayapenda mtini akasogea
Mtini akasogea sungura nakuambia
SIZITAKI MBICHI HIZI, sungura akagumia
naona nafanya kazi bila faida kujua
yakamtoka machozi matunda akalilia
Matunda akalilia Sungura nakuambia
Usifanye utani mkuu, kile Kiswahili tulichosoma sie enzi hizo kilikuwa kimetulia sana! Siyo sasa, wanetu hawajui tofauti ya “ndiyo” na “ndio” au “Hapa” na “apa” ama “Hicho” na “hiko”. Yaani hapa umenikuna kinoma.
Kwanza madarasa yale ya mwanzo kulikuwa na vitabu murua sana, kama kile cha Paulo na Selina (darasa la pili), Kuna hadithi za Kinango na Nzige, Heri Mimi sijasema na kadhalika. Ukija darasa la tatu ndio unakutana na akina Andunje, Nondo Mla watu, Twende Tukawinde,
Jogoo Aliyesema (hadithi ya Pazi) na Sadiki na Sikiri.
SHAIRI LA SADIKI NA SIKIRI
Sikiri mimi masikini
Uvivu wangu nyumbani
Ukiwa huu wa njiani
Nakufa hapa kwanini?
Sadiki sasa ashiba
Chakula kingi kwa baba
Nirudi tena kwa baba
Nakufa hapa kwanini?
Pia kitabu hiki kilikuwa na shairi la kuukaribisha mwenge, kama kuna mtu analikumbuka basi si vibaya akatukumbusha
Ukija Darasa la Nne ndio unakutana na Kibanga Ampiga Mkoloni, Ndoto ya Kimweri (chifu wa Wasambaa), Mkwawa Shujaa, Barua Kwa Mjomba Mndolwa na Siku ya Gulio Katerero (hadithi ya Kiiza). Shairi la kitabu hiki linaanza hivi:
KAMA MNATAKA MALI
Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali
Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili
Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali
Wakataka na kauli iwafae maishani
Akatamka mgonjwa, ninaumwa kweli kweli
Hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali
Roho naona yachinjwa, Kifo kimenikabili
Kama mnataka mali, mtayapata shambani
Darasa la tano napo kulikuwa na mahanjamu yake. Nakumbuka hadithi kama ile ya ‘Safari Yenye Mkosi’, Vijana Wapiga Kambi Ngulwi, Ukakamavu, Kapulya Mdadisi, nakadhalika.
SHAIRI LA KITABI HIKI LINAANZA HIVI
Tumeizika elimu, elimu ya kizamani
Elimu ile haramu, maana ya kikoloni
Imetuishia hamu, kuiga ya ugenini
Elimu yetu ya sasa yawafaa wananchi
Kitabu cha Kiswahili cha darasa la sita sikikumbuki vizuri, tulikuwa na mwalimu bomu sana ila nitajitahidi kukumbuka, nadhani kulikuwa na mada moja inahusu ‘walowezi’.
Kwa upande wa darasa la saba mambo yalikuwa poa sana. Kulikuwa na mada kama, Chuo Kikuu, Brown Ashika Tama, Jiji la Dar Es Salaam nk. Kulikuwa na mashairi mawili katika kitabu hiki, moja linaanza hivi:
Ninaye ndege mzuri, mrembo wa Kupendeza
Rangi zake mashuhuri, ni nne nawaeleza
Ndizo rangi za fahari, urembo kuutimiza
Ndege huyu ndege gani, hapa Kwetu Tanzania?
 
Dah,jamani hii story nilikuwa naichukulia kwa tahadhari sana, maana enzi hizo nilikuwa najua ni story ya kweli,that nilikuwa nachukua precuations zote linapokuja suala la mifugo hasa kuku
 
Huyu ni Baba,
Baba ni Mnene,
Baba ana ng'ombe wake,
Ng'ombe wake ni mweusi,
Baba anasema,
Kimbia Ng'ombe, Kimbia Upesi,
Baba ana njaa.
 
Huyu ni Baba,
Baba ni Mnene,
Baba ana ng'ombe wake,
Ng'ombe wake ni mweusi,
Baba anasema,
Kimbia Ng'ombe, Kimbia Upesi,
Baba ana njaa.
mkuu hiki kitabu naweza kukipata wapi? ndicho nlichojifunzia kusoma
 
Asante, umenikumbusha mbali!, nadhani hiki ni kitabu cha "Someni Bila Shida-3" Someni kwa Furaha" ndio vilikuwa vile vya darasa la kwanza na la pili, vya "JUMA NA ROZA".
Not sure anymore!.
Pasco

Kaka Pasco sasa utakiri kuwa mitaala ya sasa ni majanga
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Bujibuji fanya editing kidogo,aliyekuwa analialia ni Sikili,mdogo wake aliyekuwa anakula bata home ni Sadiki.

Sangomwile asante mkuu, mods wesha rekebisha. Unajua hizi zama zetu za kufanya shopping kwenye maduka ya Ushirika, RTC na kwenye maduka ya vijiji vya ujamaa. Umri umenitupa mkono ati
 
Last edited by a moderator:
Huyu ni Baba,
Baba ni Mnene,
Baba ana ng'ombe wake,
Ng'ombe wake ni mweusi,
Baba anasema,
Kimbia Ng'ombe, Kimbia Upesi,
Baba ana njaa.

Kuna dogo aliambiwa atunge sentensi yenye neno ng'ombe ndani yake. Dogo akakurupuka "BABA ni ng'ombe"
 
Chilunda apambana na chui, kibanga ampiga mkoloni, jogoo aliyesema, andunje. Hivi sikuhizi wanasoma vitabu gani. Good old days!
 
vitabu vya jogoo la pazi
nondo mla watu
juma na uledi
kibuyu cha babu
kwenda shuleni umebeba bagia kwenye kaptula alafau wa hujali,kwenda kujipanga barabarani kumpokea nyerere,kuimba wimbo wa chipukizi
vijana mpoo, tupoo
tupo kabisa, jeuli ya chama
chini ya umoja wa vijana wa ccm yeba waa. elimu ya zamani iliwaunganisha watanzania sio hii ya sasa ya kuwaita watoto zetu makapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…