Siku hizi haki ya mtu ni pesa na usipokuwa na pesa huna haki hata ya kuishi tanzania

Siku hizi haki ya mtu ni pesa na usipokuwa na pesa huna haki hata ya kuishi tanzania

3MMANUEL

Member
Joined
Nov 7, 2012
Posts
14
Reaction score
1
jamani wana jamii naombeni msaada wa kisheria ilikuwa mwezi wa kumi na mbili mwaka 2010 mdogo wangu alifariki dunia baada ya kuchomwa kisu na jambazi na kufanikiwa kunyang'anywa pikipiki,tuliendelea kufanya upelelezi tukafanikiwa kumkamata mtu akitumia ile pikipiki na kumfikisha polisi tangu mwezi wa 2/2011 kila tukifuatilia ile pikipiki mara tunaambiwa yule jamaa aliyekamatwa amemtaja mtu mwingine kuwa ndiye muhusika wa hilo tukio na polisi mbele yetu wamekiri kuwa wameshindwa kumkamata aliyetajwa wakatuomba sisi ndo tuwasaidie kumkamata wakati hatumjui pia wakati mwingine wanatueleza kuwa ofisi yao haina mashine ya photocopy kwa ajili ya kutolea copy zile nyaraka za kesi isitoshe wanataka tuwakabidhi kadi original ya pikipiki.naomba msaada wenu wa kisheria pamoja na ushauri.
 
haya mambo huwa yananiumiza sana kwa kweli pole sana ndugu yangu kwakumpoteza nduguyako ,ngoja wanasheria watakuja nakukupa mwongozo kwa kweli
 
wanajamii nisaidieni mwenzenu ktk hili!
Nenda legal and human right ccentre,wako pale nyuma ya chuo cha ustawi wa jamii maeneo ya sayansi dsm. Kama hauko darr tafuta website yao utapata jinsi ya kuwasiliana nao. Huwa wanatoa msaada mzuri tu wa kisheria
 
Usiwape kadi orijino,wape kopi.Ni kweli legal and human rights centre wanatoa bure msaada wa kisheria,watakusaidia sana katika hili,pole sana kiongozi.
 
Back
Top Bottom