Siku Muafrika alipoacha dini na Mungu wake ndipo shida ilipoanza?

Siku Muafrika alipoacha dini na Mungu wake ndipo shida ilipoanza?

realpatriot

Senior Member
Joined
May 28, 2009
Posts
116
Reaction score
76
Heri ya sikukuu ya noeli wadau wote na haswa wana jukwaa,
Najua wengi wetu tumepumzika,napenda kuwapa machache ambayo ukiyaangalia ni kama yana ukweli.

Afrika kama ambavyo mabara mengine huko nyuma kabisa kabla ya ukoloni na kabla ya wanaojiita wastaarabu kuja kwa ajili ya kutufundisha ustaarabu tulikua na maisha ambayo yalipangiliwa katika misingi mbalimbali kwenye kila jambo mfano shughuli zote zilipangiliwa kutokana na jinsia na rika kutokana na jamii husika pia suala la kuomba ama kusali lilifanyika barabara kulingana na jamii husika na mambo yalienda sawasawa.

Tukiangalia kwa undani baadhi ya jamii ambazo kwa asilimia kubwa mpaka leo bado ziko na tamaduni zao na bado kwa asilimia kubwa zinaendele kuabudu miungu yao na kwamba ni kwa kiasi kidogo sana wamechukuliwa na miungu ya magharibi na mashariki wamepiga hatua kubwa za kimaendeleo..

Asia, kwa mfano mpana wao wanaongoza na ukiangalia kuna baadhi ya nchi ambazo zilikua nyuma hata ya zaidi ya baadhi ya nchi barani africa zilikuja zikapita nchi nyingi na sasa ni kinara wa uchumi

Je ni kweli kwamba tungeendela na mila,mungu na tamaduni zetu bila kufuata mungu wa mashariki na mungu wa magharibi tungekua tumepiga hatua kubwa?

Je ni kweli kwamba mila potofu kama kukeketa na zinginezo tungeziacha kadri muda na elimu ambavyo ingeelea kutolewa?

karibuni tuchangie mawazo yetu..ANGALIZO TUWEKE UDINI PEMBENI NA TUJADILI KWA MAPANA
 
NIDHAMU,KUJITAMBUA,UZALENDO.

Tukijuwa kuvitumia hivi vitu vizuri tutafika mbali Sana Ahsante.
 
Kutokana na upumbavu wako ukaona maendeleo ya afrika yanacheleweshwa na dini na wewe ukaja hadharani bila aibu ukaandika eti watu waone huo upumbavu uliojuza kichwani
kisha ukajiona una akili kuliko watu wote humu
waafrika sijui tunakosea wapi
hizo ncho usizozitaja ambazo zilikua nyuma yetu sasa hatuwezi kuzifikia hazijafika zilipo kwa ajili ya dini bali kwa ajili ya sera bora za nchi zilitokelezeka

nb:upumbavu sio tusi ni kukosa maarifa
ndio maana wahenga walisema
mpumbavu akirevuka mwerevu yupo mashakani
muda upo utaondoa huo upumbavu kijana
 
Kutokana na upumbavu wako ukaona maendeleo ya afrika yanacheleweshwa na dini na wewe ukaja hadharani bila aibu ukaandika eti watu waone huo upumbavu uliojuza kichwani
kisha ukajiona una akili kuliko watu wote humu
waafrika sijui tunakosea wapi
hizo ncho usizozitaja ambazo zilikua nyuma yetu sasa hatuwezi kuzifikia hazijafika zilipo kwa ajili ya dini bali kwa ajili ya sera bora za nchi zilitokelezeka

nb:upumbavu sio tusi ni kukosa maarifa
ndio maana wahenga walisema
mpumbavu akirevuka mwerevu yupo mashakani
muda upo utaondoa huo upumbavu kijana

mkuu ambaye sio mpumbafu.....hili ni swali yafaa unijibu kutokana na maarifa yako
 
Kutokana na upumbavu wako ukaona maendeleo ya afrika yanacheleweshwa na dini na wewe ukaja hadharani bila aibu ukaandika eti watu waone huo upumbavu uliojuza kichwani
kisha ukajiona una akili kuliko watu wote humu
waafrika sijui tunakosea wapi
hizo ncho usizozitaja ambazo zilikua nyuma yetu sasa hatuwezi kuzifikia hazijafika zilipo kwa ajili ya dini bali kwa ajili ya sera bora za nchi zilitokelezeka

nb:upumbavu sio tusi ni kukosa maarifa
ndio maana wahenga walisema
mpumbavu akirevuka mwerevu yupo mashakani
muda upo utaondoa huo upumbavu kijana
Mkuu umemkosea mtoa mada hii ni intelejesia na c jukwaa la siasa au mmu hapa huwa naona mara nying kila swal Au hoja ya member huheshimiwa na hujibiwa kwa ufasaha na umakn pia mtoa mada hueleweshwa kwa busara asante
marongota
 
Sidhani kama tamaduni/ dini za asili za Afrika na miungu ya kiafrika ingesaidia/inaweza kusaidia kukua kwa Afrika.
Na sidhani kama dini na tamaduni za kigeni ndio zimesababisha African backwardness.
KWANINI
1.tamaduni nyingi za kiafrika hazina msaada katika maendeleo ya Afrika kwa mfano kuua mapacha, ukeketaji,kutoa watu kafara na ushirikina haya yote hayana msaada katika maendeleo ya Afrika.
2.Kumbuka kipindi waafrika wanatunza tamaduni zao na kumuabudu mungu wao haikuwasaidia wote kupata maendeleo na kustaarabika ila tu northen,west and some parts of east Africa,lakini watu wa central Afrika na large part of east Afrika walikuwa poor and uncivilised mfano hadzabe, khoikhoi and sans japo walitunza tamaduni zao na kuabudu miungu yao.
3.Kuhusu dini na tamaduni za kigeni zimechangia ukuaji wa kimaendeleo kwa baadhi ya falme za kiafrika mfano uislamu ulichangia kukua kwa maendeleo ya Mali,Ghana na Songhai.
Oyo kingdom walishika tamaduni zao na mungu wao lakini hawakupata maendeleo yoyote.
Kesi nyingine?
 
Sasa tutaendeleaje kama watu tupo milioni 54, lakini mtu mmoja tu ndio anaamua cha kufanya, mawazo ya watu wengine hayatumiki, labda huyo mtu mmoja apende.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Write your reply...
tumepotoka sana kwa kufuata njia za wazungu, Mimi binafsi ninaamini kua msingi wa maarifa ni elimu na msingi wa maendeleo ni maarifa. hivyo basi pamoja na elimu kuanzia afrika misri lakini bado elimu ilienezwa na wazungu, elimu iliotolewa na wakoloni ilikua ni kwajiri ya kutengeneza watu wa kuwasaidia kutawala ndio maana hata lugha zilizotumika zilikua za kwao kwajiri ya kurahisisha mawasiliano. baada ya nchi zetu kupata Uhuru tukaendelea na mfumo wa elimu ule ule kwahiyo tumekua wasaidizi mpaka kesho. kumbe ilibidi baada ya kuwafukuza wakoloni tutumie faida ya elimu tulioachiwa kubuni mfumo wa elimu ambao utaendana na mazingira yetu, tamaduni zetu, jinsi ya kutumia rasilimali zetu kujirahisishia maisha au kujiletea maendeleo kwa mfano badala ya kutumia mabomba kusafirishia maji tungeweza kutumia mianzi lakini baada ya mianzi kutuonyesha dira tungekua tunaboresha polepole kupata njia bora zaidi. tungeanza na teknolojia ya kutumia vitu vya asili leo Nina imani tungekua mbali sana kiteknolojia na maendeleo, sasa tumalaza akilli zetu, kila kitu tunategemea wazungu, mpaka tafiti za maendeleo yetu zinafanywa na wazungu. TUMEPOTOKA SANA
 
  • Thanks
Reactions: UCD
79fb7ab96bd8cf6327b1cef533d3fb9e.jpg
 
Kutokana na upumbavu wako ukaona maendeleo ya afrika yanacheleweshwa na dini na wewe ukaja hadharani bila aibu ukaandika eti watu waone huo upumbavu uliojuza kichwani
kisha ukajiona una akili kuliko watu wote humu
waafrika sijui tunakosea wapi
hizo ncho usizozitaja ambazo zilikua nyuma yetu sasa hatuwezi kuzifikia hazijafika zilipo kwa ajili ya dini bali kwa ajili ya sera bora za nchi zilitokelezeka

nb:upumbavu sio tusi ni kukosa maarifa
ndio maana wahenga walisema
mpumbavu akirevuka mwerevu yupo mashakani
muda upo utaondoa huo upumbavu kijana
Ila kanena

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom